Chemba. Katibu Tawala wa Wilaya ya Chemba mkoani Dodoma, Dorah
Makinga amelitaka Jumuiko la Maliasili Tanzania (TNRF), kuwaelimisha
madiwani matumizi bora ya ardhi ili wakawaelimisha wananchi katika ngazi
za vijiji na vitongoji.
Makinga aliyasema hayo katika warsha ya
kuzungumzia matumizi bora ya ardhi sambamba na kupatiwa ripoti ya
utafiti uliofanywa na TNRF katika Tarafa ya Kwamtoro wilayani hapa.
Alisema migogoro ya ardhi imekuwa chanzo cha kurudisha nyuma maendeleo
ya wananchi.
“Nawaomba mpange bajeti ya kuwezesha kufanya
mafunzo kwa viongozi wetu kuanzia ngazi ya vitongoji, vijiji na wilaya
ili wajue nini chakufanya wanapokutana na migogoro ya ardhi kwenye
maeneo yao.
Mratibu TNRF, Godfey Massay alikiri kuwapo kwa
migogoro mingi ya ardhi katika tarafa hiyo kutokana na utafiti
uliofanyika na kutoa wito kwa viongozi wa Serikali na wale wa siasa
kutoa ushirikiano ili kuitatua.
“Hii ni hatua ya mwanzo katika mradi huu wa ardhi,
tumefanya utafiti wa mwanzo na kugundua Tarafa ya Kwamtoro inakabiliwa
na changamoto nyingi katika ardhi, ikiwamo ya ardhi kutopimwa, hakuna
mipango ya matumizi ya ardhi, wakazi wengi hawana hati hata ya kimila ya
kumiliki ardhi,” alisema Massay.
Alisema licha ya changamoto hizo, bado eneo hilo
hukumbwa na uvamizi wa wageni wanaoingia na kujenga makazi bila kufuata
utaratibu.
Diwani wa Kata ya Farkwa, Selemani Gaawa alisema:
“Ni bahati kubwa nyie kutufikia katika kipindi hiki kutokana na hali
halisi iliyoko katika maeneo mengi ya tarafa hizi.
Ni juzi tu tumetoka kupambana na wahamiaji ambao
walisababisha baadhi ya wenyeji hapa kupoteza maisha kutokana na
kugombea ardhi.”
- Mwananchi
- Mwananchi
إرسال تعليق