Stori: MAYASA MARIWATA DUNIA HAINA HURUMA!
Mwanamama mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Sarah Lyimo, mkazi wa
Buza Mwang’ati jijini Dar es Salaam amejikuta kwenye wakati mgumu baada
ya mumewe aitwaye Mohammedi kumkimbia baada ya kile alichodai kuwa na
mtoto mwenye ulemavu.
Akifafanua zaidi Sarah alisema: “Mwanzoni tulipendana sana na mume wangu. Mtoto huyu nilipomzaa alikuwa hana tatizo lolote, alianza kukumbwa na matatizo kwa kuumwaumwa akiwa na miezi sita ndipo akaanza kubadilika na kupatwa na ulemavu wa miguu na mikono.
“Eti ndugu wa mume wanasema kwa kuwa tumempa jina la marehemu babu yake bila ridhaa ya bibi yake ambaye yupo hai ndiyo maana mtoto amelemaa, wakaniambia inabidi twende kaburini tukamuombe radhi (babu yake) ndipo mtoto atapona. Mimi sina imani hizo.
Alisema kutokana na ugumu wa maisha alionao anadhani bora arudi kwao Moshi, kuliko kuendelea kuteseka kwenye jiji asilolifahamu vizuri.
Sarah Lyimo akiwa na watoto wake.
Akizungumza na mwandishi wetu wiki iliyopita kuelezea mkasa mzima wa
kutelekezwa kwake, Sarah alidai aliishi na mwanaume huyo ambaye ni
dereva wa bodaboda kwa miaka minne na kufanikiwa kuzaa naye watoto
wawili hapa Dar.Akifafanua zaidi Sarah alisema: “Mwanzoni tulipendana sana na mume wangu. Mtoto huyu nilipomzaa alikuwa hana tatizo lolote, alianza kukumbwa na matatizo kwa kuumwaumwa akiwa na miezi sita ndipo akaanza kubadilika na kupatwa na ulemavu wa miguu na mikono.
“Eti ndugu wa mume wanasema kwa kuwa tumempa jina la marehemu babu yake bila ridhaa ya bibi yake ambaye yupo hai ndiyo maana mtoto amelemaa, wakaniambia inabidi twende kaburini tukamuombe radhi (babu yake) ndipo mtoto atapona. Mimi sina imani hizo.
Sarah Lyimo akiwa na mtoto wake aliyepata ulemavu.
“Balaa lilizidi siku hadi siku kwa baba yake kutomjali mtoto huyo kwa
matunzo yoyote na kunikashifu akidai eti mtoto wake hawezi kuwa kilema,
hata hivyo tulikuwa tukiishi kwa tabu nikapata mimba na mwanzoni mwa
mwaka jana nikaenda kujifungulia kijijini kwetu Moshi, niliporudi
nikakuta anaishi na mwanamke mwingine, ndipo aliponiacha na sasa
nimebaki nahangaika, pa kuishi sina naishi na wanangu kwa marafiki,
amenitelekeza.” Alisema kutokana na ugumu wa maisha alionao anadhani bora arudi kwao Moshi, kuliko kuendelea kuteseka kwenye jiji asilolifahamu vizuri.
Sarah Lyimo akisikitikia uonevu aliofanyiwa na mume wake, Mohammedi.
“Nawaomba Watanzania wanichangie fedha ya nauli ya kurudi kwetu pia
waniwezeshe mtaji ili nikaanzishe mradi wa kujikimu kimaisha na
wanangu,” alisema Sarah.Wakati Uwazi linakwenda mitamboni, Sarah alisema
mtoto huyo amefariki dunia Ijumaa iliyopita.
Post a Comment