Huyu ni wa pili kunaswa na kamera akimpiga mtoto…

overt-bullet-camera 
Kwa wale wazazi ambao ni wanajishughulisha na kazi mbalimbali hivyo kujikuta wakilazimika kutafuta wasichana wa kazi ili wawasaidie majukumu ya kubaki na watoto nyumbani, mshtuko mkubwa Duniani uliibuka huku kila mzazi ambaye huwa anamuacha mtoto na msichana wa kazi nyumbani kujiuliza juu ya usalama wa watoto wao kutokana na kitendo cha msichana mmoja kumpiga na kumuumiza mtoto na ushahidi wa kitendo hicho kupatikana kwenye kamera iliyotegeshwa bila yeye kujua.
Hiyo ilikuwa ni ya kutoka Uganda, kituo cha Citizen TV cha Kenya kimeripoti tukio jingine linalofanana na hilo ambapo msichana mmoja amefikishwa Mahakamani pia baada ya kurekodiwa na kamera akimpiga mtoto mdogo wa miaka mitatu na kumuumiza.
Msichana huyo Janeth Muthoni Karanja alikubali kufanya kosa hilo, kesi yake itaendelea siku ya Jumatano, huku yule msichana wa Uganda kesi yake kuendelea kusikilizwa Jumatatu ya wiki ijayo, Desemba 08.
Unaweza kuisikiliza hapa Ripoti ya taarifa hiyo ambayo nimekurekodia wakati ikirushwa hewani nakituo cha Citizen TV.

Post a Comment

أحدث أقدم