Jeshi la Polisi laingilia kati baada ya wananchi kushindwa kupiga kura Vingunguti jijini Dar es Salaam.


Jeshi la Polisi kikosi cha kutuliza ghasia kimelazimika kuingilia kati ili kulinda usalama baada ya wananchi wa vingunguti kushindwa kupiga kura katika uchaguzi wa serikali za mtaa kwenye kituo cha kata ya Mtambani kutokana na Kukosekana kwa baadhi ya karatasi za kupigia kura.
ITV imefika katika kituo hicho  kilichopo katika ofisi ya afisa mtendaji kata ya Mtambani na kukuta mamia ya wananchi wakihamasishana kwa nyimbo mbalimbali huku, huku mmoja wa wananchi hao akishilikiwa na jeshi la Polisi kutokana na kukutwa na karatasi za kupigia kura ambapo askari wa jeshi la Polisi wengine wakiwa juu ya magari yao na wengine wakizuia watu kuingia ndani ya kituo hicho. 
 
Wakizungumza na ITV baadhi ya wananchi hao licha ya kupinga zoezi la kupiga kura kuhamishiwa siku ya jumamosi wameilalamikia serikali kwa kushindwa kuwa na mifumo mizuri ambayo ingewezesha upatikanaji wa karatasi za kupigia Kura kulingana na idadi ya watu walijitokeza kujiandisha kwa wiki moja.
 
Hali ya kuahirishwa kwa uchagzu wa serikali za mitaa imejitokeza pia katika kata ya Sharif Shamba iliyopo manispaa ya Ilala ambapo ITV imefika katika eneo hilo na kukuta kituo kikiwa kimefungwa huku kukiwa na tangazo kubwa Linalosema uchaguzi wa mwenyekiti wa serikali ya mtaa utafanyika tarehe 21 mwezi huu, ambapo baadhi ya wakazi wa maeneo hayo wakiwemo wagombea wamelalamikia kupotezewa muda baada kutokana na kufika mapema kutuoni
Hapo.
 
Aidha kufuatia vurugu zilizojitokeza katika kituo cha Kinondoni mjini na baadhi ya watu watatu wamekutwa na masanduku manne ya kupigia kura na kufanya uchaguzi kua, kamanda wa polisi mkoa wa kipolisi wa Kinondoni kamilius wambura amesema jeshi la Polisi linawashikilia watu watatu kwa mahoajiano zaidi kutokana na kukutwa na karatasi hizo.
 
Aidha katika kituo cha Mivumoni kata ya wazo Tegeta, kituo cha Mikocheni na kituo cha mtaa wa Bwawani Mwanamyamala idadi kubwa ya wananchi wamejitokeza kupiga kura bila ya kuwepo kwa tatizo lolote la vifaa huku ulinzi ukioekana Kuimarishwa katika maeneo yote ambapo baadhi ya wananchi wamewataka wagombea kukubaliana na matokeo kutokana na uchaguzi huo kufanyika kidemokrasia na kufuata kanuni.
- Itv

Post a Comment

Previous Post Next Post