Dar es Salaam. Kilio cha wadau wa uchaguzi
kimesikika hatimaye, baada ya Serikali kutangaza nia yake ya kuufanya
uchaguzi ujao wa Serikali za Mitaa wa mwaka 2019 kusimamiwa na Tume ya
Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Hayo yalielezwa jana na Waziri wa Nchi, Ofisi ya
Waziri Mkuu (Tamisemi), Hawa Ghasia kuwa hata mwaka huu, Serikali
ilikuwa imeomba NEC iusimamie lakini ikashindikana kutokana na tume hiyo
kutingwa na shughuli nyingi.
Hata hivyo, Mkurugenzi wa NEC, Julius Malaba
alishindwa kukubali wala kukataa kuhusu kuwapo kwa mpango huo
alipoulizwa jana, badala yake alisema atafutwe leo kwa ufafanuzi zaidi.
“NEC walikubali, lakini pia walitueleza ugumu wa jambo hili kwa sasa. Ni
kuhusu Daftari la Kudumu la Wapigakura wanalolitumia katika Uchaguzi
Mkuu, walisema ni ngumu kutumia daftari hilo katika uchaguzi wa Serikali
ya Mtaa,” alisema Ghasia.
Kwa muda mrefu, watu wa kada mbalimbali nchini
wamekuwa wakishinikiza Uchaguzi wa Serikali za Mitaa kusimamiwa NEC
badala ya Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo inaongozwa na wanasiasa wenye
masilahi na uchaguzi huo.
Hoja za wadau hao hazina tofauti na kasoro nyingi
za uchaguzi wa mwaka huu ambao umeahirishwa katika baadhi ya maeneo na
kugubikwa na vurugu za kutokuaminiana.
Hata hivyo, Ghasia alisema pamoja na kasoro hizo,
mwaka huu kulikuwa na mafanikio makubwa kulinganisha na uliopita...
“Mwaka 2009 mpigakura alikuwa akipewa karatasi nyeupe na kutakiwa
kuandika majina ya wagombea anaotaka kuwapigia kura, ndiyo maana
hakukuwa na lawama za kukosekana kwa karatasi za kupiga kura.”
- mWANANCHI
- mWANANCHI
إرسال تعليق