
Mtu mmoja ameripotiwa kuuawa nchini Kenya kufuatia mlipuko katika klabu moja ya usiku katika mji wa Wajir kaskazini mwa Kenya.
Kwa
mujibu wa Kamishna wa Polisi wa Wajir, Frederick Sishia, shambulio hilo
limefanyika saa mbili usiku na kuua mtu mmoja na watu wengine wanne
wamejeruhiwa.
Washambuliaji hao walitumia magruneti na silaha nyingine za kijeshi kufanya shambulio hilo.
Wiki iliyopita watu wengi waliuawa eneo la Mandera kaskazini mwa Kenya.
Kenya
imejikuta ikilengwa na mashambulio ya kigaidi tangu majeshi yake
yapelekwe nchini Somalia kukabiliana na wapiganaji wa Al Shabab. Mbali
na miji ya kaskazini mwa Kenya kushambuliwa kila mara, miji mikubwa
nchini humo ya Nairobi na Mombasa imekuwa ikilengwa na mashambulio ya
kigaidi.CHANZO:BBC
Post a Comment