Sheria dhidi ya ugaidi ya Kenya ni bora kuliko ya USA



Kiongozi mmoja wa ngazi za juu wa Kenya ameikosoa vikali Marekani na kusema kwamba sheria ya kupamabana na ugaidi ya nchini Kenya ni bora zaidi kuliko ile ya Marekani.

Matamshi ya kiongozi huyo wa Kenya yametolewa baada ya makundi ya upinzani nchini Kenya, baadhi ya nchi na mashirika ya kutetea haki za binadamu ya ndani na ya kigeni kuikosoa sheria hiyo iliyotiwa saini siku ya Ijumaa na Rais Uhuru Kenyatta. 

Jennifer Rene "Jen" Psaki Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje wa Marekani ameikosoa vikali sheria hiyo na kusema kuwa, Washington imeingiwa na wasiwasi mkubwa kutokana na kuwepo mbinyo zaidi wa uhuru wa raia kwenye sheria hiyo. 

Kiongozi huyo wa Kenya ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa, Marekani haipasi kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo, kwani sheria iliyopitishwa ya kupambana na ugaidi ni bora kuliko ile ya Marekani. 

Miongoni mwa vipengee vinavyopigiwa kelele ni sheria ya kuongezwa muda wa kushikiliwa watuhumiwa wa ugaidi kutoka siku 90 za awali hadi karibu mwaka mmoja.
Chanzo: kiswahili.irib.ir

Post a Comment

أحدث أقدم