WAPIGA KURA KIMARA KING'ONGO WAKUSANYA SAINI KUMPINGA MWENYEKITI MPYA

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimeanza kukusanya saini za wananchi wa King’ongo kupinga matokeo ya uchaguzi ambayo tayari wameandika kuyapinga kwa msimamizi wa uchaguzi  wilaya ya Kinondoni.
Tayari hadi kufikia jana saini zaidi ya 200 zimekusanywa .
Ukusanyaji wa saini hizo ambazo zinakusanywa ndani ya mtaa huo ambao upo kata ya Saranga unafanyika kutokana na msimamizi wa uchaguzi wa mtaa huo, Rebecca Rioga kudaiwa kutangaza mshindi kinyume na utaratibu.
CUF ambao walishiriki katika kivuli cha ukawa wamesema pamoja na CCM kutangazwa mshindi, hawakuwa wameshinda kwani kilichotokea ni msimamizi kukiuka  utaratibu  katika uthibitishaji wa kura.
Ushindi wa CCM ulitangazwa saa tano usiku chini ya usimamizi wa Polisi kutoka kituo cha  Mbezi.
Awali mawakala wa CUf wakati wa kuhesabu kura pamoja na ushindi waliokuwa nao waliona kuna idadi kubwa ya kura zinazozidi ambazo pia zina mfumo  mmoja wa mkunjo na kupigiwa mgombea wenyekiti  wa CCM . Kura hizo zilipata 32.
Mzozo wa matokeo ulianzia hapo kwani msimamizi alishindwa kueleza zilipotokea kura 32.
Jumla ya kura zote zilizopigwa zilikuwa 930 kati ya watu 1,364 waliojiandikisha kupiga kura, lakini idadi ya kura zote za wagombea uenyekiti ni 956 zikiwa ni kura 32 zaidi hasa baada ya kura 6 .
Katika barua ya kupinga matokeo kwa msimamizi wa uchaguzi halmashauri pamoja na kueleza bayana nini kilitokea katika uchaguzi huo pia wamesema kwamba mgombea Demetreus Mapesi wa CCM alitumia nafasi ya yeye kuwajua wasimamisi kutengeneza hila ya ushindi mwishoni.
Mapesi ni mwenyekiti wa Shule ya Msingi King’ongo ambacho kilikuwa kituo cha kupigia kura na wasimamizi pia wanatoka shule hiyo hiyo.
Katika kura kituo A waliopiga kura walikuwa 485 na kituo B waliopiga kura walikuwa  445 na kufanya jumla kuwa 930.Wagombea uenyekiti CUF Abubakari  Nyamguma kituo A alipata kura 253 na kituo B 224 ambapo mgombea wa CCM Demetreus Mapesi kituo A alipata kura 232 na kituo B 247  .
Ukijumlisha kura walizopata wagombea zinakuwa 956 na kuwa na ongezeko la kura 32.
mwisho

Post a Comment

أحدث أقدم