Wawekwa kiporo maeneo mengi

Dar/mikoani. Uchaguzi wa Serikali za Mitaa jana ulilazimika kuahirishwa katika baadhi ya maeneo nchini, kutokana ama na kukosewa kwa majina ya wagombea, baadhi yao kuwekewa nembo za vyama wasivyotoka au uhaba wa vifaa vya kupigia kura.

Mikoa iliyoripotiwa baadhi ya vijiji, mitaa na vitongoji vyake kushindwa kupiga kura ni Dar es Salaam, Manyara, Kilimanjaro, Tanga na Mwanza hali iliyozua malalamiko kutoka kwa wananchi waliojitokeza.

Waandishi wa gazeti hili waliripoti kuwa kati ya saa 4.30 asubuhi na saa sita mchana, masanduku na vifaa vingine vilikuwa havijafika katika baadhi ya vituo, hali iliyowakatisha tamaa baadhi ya wananchi hivyo kuanza kuondoka huku katika baadhi ya maeneo wakiamua kusubiri hadi kieleweke.


Dar es Salaam

Maeneo ambayo uchaguzi huo umeahirishwa katika Mkoa wa Dar es Salaam ni Mtaa wa Sharif Shamba Ilala, Gerezani na mitaa yote ya Vingunguti.

Ofisa Mtendaji wa Mtaa wa Sharif Shamba, Rose Magina alisema: “Uchaguzi umeahirishwa hadi Jumapili ijayo (Desemba 21) baada ya kukosekana kwa karatasi za kupigia kura.”

Waandishi wetu walipokuwa katika mtaa huo walikuta kituo cha kupigia kura kikiwa kimefungwa, huku kukiwa na tangazo linaloeleza tarehe ambayo uchaguzi utafanyika.

Katika mitaa ya Gerezani Mashariki na Gerezani Magharibi, ambako baadhi ya watendaji waliokuwa katika Ofisi za Kata ya Gerezani walisema vifaa vilivyotolewa vilikuwa vichache kuliko idadi ya watu waliojiandikisha na kwamba uchaguzi huo utafanyika tena Desemba 20, mwaka huu.

Uchaguzi pia uliahirishwa katika mitaa yote ya Kata ya Vingunguti baada ya kikao kilichowahusisha wagombea wote, huku Ofisa Mtendaji Kata hiyo, Protas Tarimo akisema utafanyika Jumapili ijayo.

Mitaa hiyo ni Miembeni, Butiama, Mji Mpya, Mtakuja, Majengo, Kombo, Mtambani na Faru. Wagombea wa vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), walimtupia lawama ofisa mtendaji huyo kwa kukubali kupokea karatasi za kupigia kura zikiwa pungufu na kusababisha uchaguzi huo kuahirishwa.
Wakazi wa Mtaa wa Machimbo, Ugombolowa, Segerea nao walikumbana na sintofahamu hiyo baada ya kufika katika kituo cha kupigia kura alfajiri, lakini mpaka saa nne asubuhi hakukuwa na dalili zozote
- Mwananchi

Post a Comment

Previous Post Next Post