Zilivyokuwa siku tisa za sakata la Escrow

 
Dar es Salaam. Watanzania kila kona walikuwa wakifuatilia mwenendo wa Bunge, licha ya kukatika kwa umeme kutokana na hitilafu zilizokuwa zikijitokeza.
Zifuatazo ni siku tisa muhimu za sakata la uchotwaji wa fedha katika Akaunti ya Tegeta Escrow, lililoibuliwa bungeni na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila kabla ya Kamati ya PAC inayoongozwa na Kabwe Zitto kulifanyia kazi, baada ya taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG).
Novemba 22
Moto wa kashfa ya ufisadi katika akaunti ya Tegeta Escrow unaoendelea kuwaka bungeni, sasa unaonekana kugeuka gharika inayoweza kuwakumba vigogo wengi zaidi na kuiweka Serikali ya Rais Jakaya Kikwete katika hali ngumu.
Kashfa hiyo ya uchotaji wa Sh306 bilioni za akaunti ya Escrow, inahofiwa kuwakumba vigogo zaidi ya 50 ndani ya Serikali wakiwamo mawaziri, makatibu wakuu, wabunge, majaji na wakuu wa taasisi za Serikali.
Habari zilizopatikana zinaeleza kuwa kutokana na kuwapo kwa idadi kubwa ya mawaziri na watendaji wa Serikali na Mahakama, hali hiyo inatishia anguko la Serikali.
Novemba 23
Hali ilikuwa tete.
Ndiyo neno ambalo unaweza kulizungumza kuhusu kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow.
Mji wa Dodoma ulikuwa umejaa pilikapilika zikiambatana na mikutano iliyokuwa ikijadili kashfa hiyo.
Kamati ya Uongozi wa Bunge, Kamati ya Uongozi wa Wabunge wa CCM na Baraza la Mawaziri, kwa nyakati tofauti walikaa kujadili ripoti ya Escrow ambayo ilijadiliwa na Bunge Jumatano na Alhamisi wiki iliyopita.
Kikao cha wabunge wa CCM kilifanyika kujadili suala hilo. Wabunge walionekana kila kona ya Viwanja vya Bunge jana wakijadiliana katika vikundi kuhusu sakata la escrow, huku wengine wakitaka hata miswada yote iliyobaki isijadiliwe ili kutoa nafasi kuichambua kwa kina kashfa hiyo.
- Soma Zaidi Mwananchi

Post a Comment

Previous Post Next Post