AY amwagia sifa ex-girlfriend wake Amani wa Kenya

Msanii wa muziki na mfanya biashara Ambwene Yessaya a.k.a AY yuko jijini Nairobi kwa sasa, na katika moja ya mahojiano aliyoyafanya na Standard Digital ya Kenya, amezungumzia uhusiano wake na ex-girlfriend wake mwimbaji wa Kenya Amani ulivyokuwa.

Katika mahojiano hayo AY amemsifia Amani kwa kusema kuwa katika miaka mitatu ya uhusiano wao, Amani alimfundisha jinsi wanawake wa Kenya walivyo na misimamo iliyonyooka katika mambo yao, na kuongeza kuwa Amani hakuwahi kuchanganya biashara na starehe.

“During the three years we dated, Amani showed me how Kenyan women are the most straight-forward in the world. Not one time did she ever mix business with pleasure,” Alisema AY

Source: SDE

Post a Comment

Previous Post Next Post