Dar es Salaam. Ni usiku na giza limetanda.
Nakatiza mitaa ya Buguruni Madenge na Malapa jijini Dar es Salaam,
nashuhudia wanawake wamejilaza kwenye vibaraza, mbele ya nyumba zao
wakitumia mwanga wa vibatari.
Akili inanikumbusha simulizi zilizoenea mjini
kuhusu kuwapo wanawake wanaojiuza kwa mtindo huo na baada ya kuchunguza,
nabaini ukweli kwamba hao waliojilaza, wapo kazini wakisubiri wateja wa
biashara ya ngono. Wanawake hao wa makamo, wengi wakiwa na umri wa
kuanzia miaka 15 na hadi zaidi ya 35, huanza shughuli hiyo baada ya jua
kuzama, pia wanatoa huduma hiyo hata wakati wa mchana bila kujali kuwa
wanachofanya ni kosa kisheria.
Wanawake hao ni sehemu ya maelfu ya wanawake wengi wanaojihusisha na biashara hiyo haramu jijini Dar es Salaam.
Ingawa hakuna takwimu sahihi kuhusu idadi ya
wanawake wanaofanya biashara hiyo, ukweli ni kwamba wanawake hao,
maarufu kama machangudoa au madada poa, wametapakaa maeneo mengi jijini
Dar es Salaam.
Maeneo yanayosifika kwa biashara hiyo ya ukahaba
ya madanguro ni pamoja na Mwananyamala, Tandika, Temeke, Keko, Buguruni,
Mbagala na Sokota.
Taarifa zinaonyesha kuwa kwa danguro la Sokota,
wanaotafuta wanawake kwa ajili ya ngono hawahitaji kuumiza vichwa
kutokana na kuwapo kwa kundi kubwa la mabinti ambao huvalia mavazi ya
aibu, wakiwa nusu utupu, hali ambayo wanaamini kuwa huvutia wateja wao.
Hata hivyo, mamlaka husika zimeshindwa kudhibiti vitendo hivyo kwani hajizachukua hatua stahiki kukomesha hali hiyo.
Mwaka 2013, Jeshi la Polisi Kinondoni lilitangaza
kufunga madanguro yaliyopo Mwananyamala na kuwakamata wasichana 35
waliokuwa wakiuza miili yao pamoja na mama wa miaka 72 ambaye anadaiwa
kuwa ndiye mmiliki wa madanguro hayo na kuwafikisha mahakamani.
Hata hivyo, baadhi ya madanguro hayo, yamefunguliwa na kina dada poa wanaendelea kufanya kazi.
Uchunguzi wa gazeti hili katika baadhi ya maeneo
umebaini wanawake hao wamekuwa wakiwatoza wateja wao ya Sh3,000 hadi
Sh5,000 kwa tendo moja la ngono.
Hata hivyo, bei zinatofautiana na huwa kubwa zaidi
kwa wale wanaofanya ngono kinyume na maumbile. Ukiondoa wanaume
wakware, uchunguzi umebaini wanafunzi nao ni wateja wazuri wa wanawake
hawa.
Kuna aina mbili za wanawake wanaouza miili yao.
Kundi la kwanza ni la wale wanaoendesha biashara hiyo katika vyumba
maalumu walivyopanga mitaani na jingine ni la wazururuaji. Hawa
huonekana wakirandaranda barabarani, hasa nyakati za usiku wakitega
wateja au katika klabu za pombe na nyumba za wageni maarufu kwa kazi
hiyo.

إرسال تعليق