Hii Ndio U Heard ya leo Jan 09 iliyosikika kwenye XXL ya Clouds FM, inamhusu Sheikh Sharif

Kwenye Uheard ya leo Jan 9, Soudy Brown amezungumza na Sheikh Sharif ambaye alitoa taarifa kuwa kuna ndoto aliyoota ambayo ni ujumbe kwa Tz, akitolea ufafanuzi ndoto hiyo Sheikh Sharif amesema alipotafsiri ndoto hiyo aliweza kupata mambo saba ambayo yatatokea kwa mwaka 2015.
Baadhi ya mambo aliyotolea  tafsiri ni pamoja na kunyesha kwa mvua  kubwa itakayoleta mafuriko, chombo kikubwa kuzama Baharini na  kufariki kwa kiongozi mkubwa kati ya wale waliotangaza nia ya kugombea Urais,  ambaye amemtaja kwamba anakubalika sana ingawa hajajua  ni wa chama gani na wala kifo chake kitatokana na nini.
Sheikh sharif ameseama amewahi kuota mambo kadhaa siku za nyuma ambayo yalitokea ikiwemo Rais Uhuru Kenyatta kuwa Rais wa Kenya,  kuzama kwa meli ya Mv Bukoba na  yote yalitokea, hivyo ameamua kulisema hili ili watu wachukue tahadhari.
Unaweza kuisikiliza kwa kubonyeza play

Post a Comment

أحدث أقدم