MREMBO ANASWA AKICHANGISHA MICHANGO

MREMBO mmoja aliyefahamika kwa jina la Regina Thobias (29) amenaswa akitapeli watu kwa kuwachangisha fedha akidai kuuguliwa na mgonjwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Iringa, kitu ambacho siyo kweli.
Tukio  hilo lilitokea Ijumaa baada ya  mrembo huyo anayeishi eneo la Frelimo mjini hapa, kutaka kumtapeli dereva wa halmashauri ya mji, akiomba asaidiwe fedha ili akalipie hela za matibabu kwa shangazi yake aliye hoi hospitalini hapo.
Hata  hivyo dereva huyo hakuweza  kutoa  fedha  hizo  baada ya kumshuku kuwa tapeli, lakini wakati akitafakari, ghafla binti huyo aliondoka na kwenda kupanga foleni kama mtu anayetaka kuchukua fedha katika mashine za ATM ya benki moja iliyopo eneo hilo.
Lakini kama ilivyo kawaida za mwizi ni 40, baadhi ya  watu  waliopata  kutapeliwa na mrembo huyo walianza kumhoji kwa kitendo chake cha kupanga foleni katika  ATM  kwani kwa wanavyomjua, asingeweza kuwa na akaunti. Hata walipomtaka kuonyesha kadi yake alishindwa.
Wakizungumza eneo la tukio, baadhi ya waliopata kutapeliwa naye walisema mrembo huyo amekuwa na tabia ya  kutapeli watu mbalimbali  kwa  kuwadanganya kuwa ana mgonjwa  Hospitalini na yeye anaishi  Ilula, kwamba  ameporwa  pesa  zake na  vibaka.
Akijitetea, binti huyo alikiri kufanya vitendo hivyo kutokana na hali ngumu ya maisha. Akaomba kusamehewa, wakamwachia kwa sharti kuwa asirudie tena tabia hiyo

Post a Comment

أحدث أقدم