Muigizaji Angelina Jolie akutana na papa Francis

Alhamisi wiki hii mwanadada ambaye yuko juu katika uigizaji Angelina Jolie alikutana na kiongozi wa kanisa katoliki, Papa Francis baada ya kumalizika kuonesha filamu yake ya Unbroken.
Mdada huyo ambaye ameshajitwalia tuzo kadha za Oscar ndiye aliyeiongoza sinema hiyo ambayo inamzungumzia Louis Zamperini,shujaa wa vita kuu ya pili ya dunia.
Filamu hiyo ya Angelina Jolie ilioneshwa kwa wakazi wa Vatican. Lakini mkazi namba moja, Papa Francis hakuweza kuiona.
Imeelezwa kuwa papa alikutana na Angelina Jolie kwa faragha kwenye kasiri la kitume  mume wa Jolie, Brad Pitt hakuwepo.
Jolie alisema kupewa nafasi ya kuonesha filamu hiyo Vatican ni heshima tosha na inaonesha kwamba Louiewa kupigiwa mfano katika masuala ya kusamehe.


Mkutano wake na Papa umefanyika  miezi miwili baada ya kukaribishwa na malkia wa Uingereza,Elizabeth II kupewa tuzo ya heshima ya Order of St Michael and St George .
Amepewa heshima hiyo kutokana na juhudi zake za kukabiliana na unyanyasaji wa kijinsia na mchango wake katika siasa za nje za Uingereza.
Mwisho

Post a Comment

Previous Post Next Post