![]() |
| hali ya mwanamke na jamaa pembeni |
MWANAUME mmoja nchini Nigeria ametembeza mkong’oto kwa
mke wake wa ndoa kwa kumi na mitano kisa amezungumza na mchungaji.
Kumdunda huko kunatokana na kauli
aliyompa ambayo ilimkataza mwanamke huyo kuzngumza na mchungaji huyo katika
kile kinachoonekana faulo Fulani inayofanywa na mumewe itajulikana.
Mwanamke huyo anadai kwamba mumewe
anatoka na mke wa mchungaji ambaye alikuwa ni rafiki yake mdada.
Mwanamama huyo ambaye anajulikana
kwa jina la Comfort Oluwaseun Adebowale, ameolewa na mtu ambaye alimsaidia
kumpeleka shule baada ya wazazi wake kufariki na ndugu zake kumwacha awe
chokoraa.
Mwanamke huyo alisema alipomsaidia mwanaume
huyo Olorode Abimbola Gbenga ambaye kwa sasa kapata kazi ya ualimu jimbo la Abeokuta
Ogun alifanya hivyo kwa mapenzi kwa kuwa
alikuwa ndiye chaguo lake, alipenda kuishi naye daima.
Comfort alimsaidia mwanaume huyo
mwaka 1999 akimlipia kila kitu shuleni.
“ Nilifanya hivi kwa kuamini kwamba
nawekeza kwa mwanaume ambaye atakuja kuwa mume wangu, nilimpenda na nilitamani
kuwa naye daima”
Lakini mambo yalianza kubadilika
mwaka 2008 wakati mwanaume huyo alipopata kazi, kwani tabia yake ilibadilika,
akawa anachelewa kurejea nyumbani, akawa anajibu simu kutoka kwa wanawake
wasiojulikana, akawa tofauti na mbaya zaidi akaanza kumpiga.
Kwa muda wote akawa anasali akimlilia
Mungu aguse moyo wake ili aweze kubadilika na kumrejesha nyumbani lakini kila kukicha afadhali ya jana.
Mume wake kwa miaka 15 akaanza
kujimwaga na rafiki wa mke wake, mtume na mke wa mchungaji katika kanisa
wanalosali la Kondoo wateuliwa wa Kristo na kanisa la miujiza (shepherd
of Christ Anointed & Miracle Church), Aregbesola Eleweran Abeokuta.
Katika mazungumzo ya simu na
mwandishi wa habari, mwanamke huyo aliyepigwa vibaya alisema kwamba mumewe na mwanake huyo walianza uhusiano wa kimapenzi
mwaka jana na katika hali ya kuogopa kwamba atawashika alimwelekeza kwamba hana
ruksa ya kumsalimia mchungaji wao Samuel Adeniji wala kumuona akizungumza naye.
Pamoja na maagizo hayo januari 3
mwaka huu akiwa anaenda sokoni alimuona mchungaji huyo akiwa katika mlango wa
kanisa lao alisimama na kumsalimia na wakati akifanya hivyo mumewe akajitokeza
na kumtandika makofi palepale na kama haikutosha akanyanyua jiwe na kutandika
nalo usoni huku akimwagia maneno (matusi) ambayo hayafai kunadikika huku
akimlaani afe.
Comfort aliachwa kwenye dimbwi la
damu na kuja kuokolewa na wasamaria
ambao walimkimbiza hospitali kwa matibabu.
Mwanamke huyo amesema kwamba
amelifikisha shauri hilo Polisi, lakini
mume wake anatumia ngao ya baba mkwe ambaye alikuwa Kamishina Msaidizi
wa Polisi Olorode Timothy ambaye amestaafu ili polisi wasimsikilize wala
kuchunguza suala hilo.
Oluwaseun Comfort Adebowale amewataka wanawake wanaopata kadhai kama yake wahakikishe
wanajinasua kabla mambo hayakuwa mabaya kama yalivyo kwake.
Oluwaseun Comfort Adebowale amesema
kwa wanaotaka kumsaidia anaptikana katika namba 08122174991 .
Mwandishi wa habari hii ni
Mwanasheria Chukwudi Iwuchukwu ambaye yuko kwenye twita akitwiti @Chukwudi1985
mwisho

Post a Comment