Mwanamuziki ataka ukahaba uwe ruksa

Mwanamuziki wa Nigeria Caroline Sam, al maarufu kama Maheeda katika duru za muziki ambaye alishawahi kuwa kahaba kabla ya kujiingiza katika muziki anataka ukahaba uwe ruksa nchini Nigeria.

 Mwanamuziki huyu ambaye anajulikana kwa kauli zake za kiutata na kuposti picha za mapenzi katika mitandao ya jamii  amesema itakuwa vyema ukahaba ukawa ruksa. Alisema yapo mataifa ambayo yamesaidia sana kuhalalisha ukahaba kama ilivyo Holand na kwamba Nigeria ikiruhusu itasaidia sana. Alisema pamoja na kupigwa marufuku uko kila mahali na unakuwa tatizo kwa hiyo uruhusiwe ili uwe na vigezo vyake na mamboi yanayoambatana na biashara kama leseni na ulipaji wa kodi kwa serikali.

Post a Comment

أحدث أقدم