Mwenyekiti CCM apata kashfa

Tabora. Mwenyekiti mmoja wa CCM wilayani Uyui, (jina linahifadhiwa) anatuhumiwa kumlawiti kijana mmoja nyumbani kwake maeneo ya Bachu baada ya kumlewesha pombe.
Kijana huyo anayefanya biashara ya kuuza chipsi eneo la Bachu, Manispaa ya Tabora anadaiwa kulawitiwa na mwenyekiti huyo wiki iliyopita kisha kuingiziwa vitu kwenye makalio yake.
Mmoja wa ndugu za kijana huyo, alikiri kwa ndugu yake kufanyiwa vitendo visivyofaa baada ya kuleweshwa pombe.
Kutokana na tukio hilo, ndugu huyo alimpigia simu mwenyekiti huyo kumuulizia kuhusu tukio hilo lakini alikana na waliamua kutoa taarifa polisi.
Alipoulizwa kuhusiana na tuhuma hizo, mtuhumiwa alikanusha kuhusika na kitendo hicho na kwamba ni mahasimu wake wa kisiasa ndiyo wametengeneza tukio hilo kwa lengo la kumchafua kisiasa.
Alisema hamfahamu kabisa kijana huyo na hawezi kufanya kitendo hicho, kwani ni kiongozi anayeheshimika kwa jamii.
“Kwanza huyo kijana kwa kweli simfahamu na haya ni mambo ya kutengenezwa na baadhi ya mahasimu wangu kisiasa,” alisema mtuhumiwa huyo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Susan Kaganda alithibitisha taarifa za tukio hilo kufikishwa kituoni na wanachunguza iwapo lina ukweli. “Taarifa hizi zimefika kwetu na sisi kila tuhuma tunaifanyia kazi,” alisema  KamandaKaganda. Taarifa kutoka ndani ya polisi zilidai kuwa maofisa wa jeshi hilo kutoka makao makuu Dar es Salaam wamewasili mjini hapa kufuatilia tukio hilo.
Baadhi ya viongozi wa CCM Wilaya ya Uyui, walikwenda polisi kufuatilia suala hilo baada ya mwenyekiti wao kukamatwa na kuhojiwa kutokana na tukio hilo.
 Mmoja wa viongozi hao ambaye hakupenda kutajwa jina lake, alisema hawapendi kuingilia suala hilo na wanaviachia vyombo vya dola vifanye kazi yake.

Post a Comment

Previous Post Next Post