Rushwa kwenye uchaguzi inavyo wanyima wananchi viongozi bora

Dar es Salaam. Akiwa na kaptula pana, tumbo wazi huku amebeba beleshi, Ally Bakari ‘Champion’, bondia wa zamani wa masumbwi na mkazi wa Mtaa wa Buguruni Kisiwani, anawaongoza wenzake kwenda kuzibua mtaro wa maji taka ambao umeziba na kuzua mtafaruku mtaani hapo.
Anafanya hivyo si kwa vingine isipokuwa ni kutokana na hulka yake ya kutokupenda kuacha mambo yakiharibika wakati uwezo wa kuyarekebisha upo.
Safari yao hiyo inafikisha eneo hilo na kwa jitihada zao wanafanikiwa kuyazuia yasitiririke katika makazi ya watu lakini hata hivyo bado yanamwagika.
Mkazi huyo anachukua hatua za ziada ikiwa ni pamoja na kuwasiliana na mafundi wa Mamlaka ya Majisafi na Taka Dar es Salaam (Dawasa), ambao wanafika na kutatua tatizo.
Tukio hilo ni moja kati ya mengine yanayomhusisha mkazi huyo, likiwamo la eneo linalodaiwa limeuzwa ambalo awali lilitengwa kwa ajili ya ujenzi wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Buguruni.
Jitihada zake hizo hata hivyo zinagonga mwamba kwani kunabainika kwa kuwa walioliuza ndiyo waliyopelekewa malalamiko hayo, kwani mwitikio hakuna.
Huyo ndiyo Championi, mwanaharakati wa maendeleo ya kijamii ambaye ili kuweza kuona anapata nafasi ya kutekeleza dhamira yake ya kuwatumikia wananchi kwa kuwashirikisha kutatua kero zao.
Ni mmoja wa watu waliomba nafasi ya uenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo wa Kisiwani kupitia Chama cha Wananchi (CUF).
Hata hivyo, anachokiona wakati wa kupiga kura kutafuta mgombea wa nafasi hiyo ndani ya chama, kinamfanya afikirie mara mbili kuhusiana na dhamira za wanasiasa kwa wananchi wanapowania nafasi mbalimbali za uongozi.
Anasema yeye ndiye aliyekuwa chaguo la wakazi wa Kisiwani kwa mapenzi yao toka moyoni na siyo kwa vishawishi vya pesa au vitu vingine vya namna hiyo.
Anabainisha kuwa siku ya upigaji wa kura mambo mengi ya ajabu yalijitokeza kwani licha ya kuongoza muda mrefu huku kila mmoja akijua kuwa yeye ndio chaguo la chama hicho, anasema alishangaa kuona wapiga kura hawaishi na mbaya zaidi vikao visivyo rasmi nje ya ukumbi.
“Wanachama waliandika barua, ofisi ya kata, wilaya hadi mkurugenzi wa Taifa wa uchaguzi anatambua hilo lakini hakuna hatua za maana ziliozochukuliwa,” anasema na kudai kuwa:

Post a Comment

Previous Post Next Post