TIMUA TIMUA YAANZA BARCELONA, Mkurugenzi wa soka Afukuzwa, Carles Puyol aachia ngazi, Kocha akalia kuti kavu

…mkurugenzi wa soka afukuzwa, Carles Puyol aachia ngazi, kocha akalia kuti kavu
Andoni Zubizarreta (pichani juu) ametimuliwa kwenye nafasi yake ya ukurugenzi wa michezo Barcelona huku msaidizi wake Carles Puyol akiachia ngazi.
Zubizarreta ambaye alishika nafasi hiyo tangu Julai 2010,  ametimuliwa na rais wa klabu hiyo Josep Maria Bartomeu na kuhitimisha tetezi za kutimuliwa kwake zilizotanda wiki nzima iliyopita.
Taarifa ya klabu imesema: “Rais wa Barcelona Josep Maria Bartomeu ameamua kusitisha mkataba wa mkurugenzi wa michezo Andoni Zubizarreta.
“Rais kwa niaba ya klabu, anamshukuru Andoni Zubizarreta kwa mchango wake, kujitoa kwake kwa miaka minne iliyopita.”
Barcelona haridhiki na mwendo wa timu na sasa itajadili hatma ya kocha Luis Enrique katika mkutano wa dharura wa bodi ya timu utakaofanyika Jumatano.


Carles Puyol aliteuliwa kuwa msaidizi wa Andoni Zubizarreta mwezi Mei 2014, muda mfupi baada ya kustaafu kusakata soka ndani ya timu hiyo.

Post a Comment

Previous Post Next Post