Uwanja wa ndege Nairobi wafungwa kwa saa kadhaa

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA) nchini Kenya umefungwa leo kwa masaa kadhaa baada ya ndege moja kulazimika kutua kwa tumbo kutokana na matairi yake kushindwa kufunguka.

Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta (JKIA)

Maafisa wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege ya Kenya wamesema kuwa, shughuli za usafiri katika uwanja huo zimezorota kwa zaidi ya masaa matano na ndege zote zikalazimika kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mombasa.

Ndege hiyo ya ndani ilikwama kwenye barabara ya kutua ndege baada ya kusimama kikamilifu. Hakuna habari zaidi zilizotolewa kuhusiana na ajali hiyo.

Wakati huo huo maafisa usalama wa Kenya wameanza kufanya uchunguzi kuhusiana na kifo cha Fidel Odinga, mwana wa Waziri Mkuu wa zamani wa nchi hiyo Raila Odinga, ambaye amekufa leo asubuhi.
Wakati huo huo salamu za rambirambi zimeendelea kumiminika nyumbani kwa Raila Odinga ambaye ni mkuu wa mrengo wa upinzani wa Cord.

Katika upande mwingine, shahidi mmoja aliyetoa ushahidi kwenye Makahama ya Kimataifa ya Jinai ICC amepatikana ameuawa huku mwili wake ukiwa una viungo pungufu.


Vyombo vya habari vya Kenya vimeripoti leo Jumapili kuwa, mwili wa Meshak Yebei ulipatikana siku ya Ijumaa baada ya kutoweka kwa muda wa wiki nzima nyumbani kwao, katika Kaundi ya Uasin Gishu, jambo ambalo limezusha wasiwasi kati ya watu wa familia na wanaharakati wa haki za binadamu.

Mwili wa Yebei ulipatikana unaelea kwenye Mto Yala katika Kaunti ya Nandi, zaidi ya kilomita 40 kutokana nyumbani kwake huko Sugoi, katika Kaunti ya Uasin Gishu.

Post a Comment

Previous Post Next Post