Polisi
nchini Ufaransa wanasema kuwa wanaume waliokuwa wamejifunika nyuso
wamewaua takriban watu 12 kwenye ofisi za gazeti moja la vibonzo la
Charlie Hebdo.
Watu wengine watano wameripotiwa kujeruhiwa vibaya.Gazeti hilo lililo mjini Paris limekuwa likilengwa na wanamgambo wa kiislamu siku za nyuma.
Polisi wanafanya msako mkubwa kuwatafuta washambuliaji huku mji wa Paris ukiwa chini ya tahadhari kubwa.
Rais wa ufaransa Francois Hollande amelaani shambulizi hilo akisema kuwa nchi hiyo imepatwa na mshangao mkubwa.
Inaarifiwa watu watano walijeruhiwa katika uvamizi huo
Inaarifiwa washambulizi walisikika kwa sauti ya juu wakisema ''tumelipiza kisasi kw aniaba ya Mtume Muhammad.'
Waandishi wanne wa jarida hilo la vibonzo, akiwemo mhariri mkuu Stephane Charbonnier walikuwa miongoni mwa waliouawa pamoja na maafisa wengine wawili.
Vyombo vya habari vimewataja wachoraji wengine watatu waliouawa wakiwemo, Cabu, Tignous na Wolinski. Duru zinasema shambulizi hilo lilifanyika wakati wa mkutano wa kila mwezi wa uhariri wa jarida hilo.(BBC)




Post a Comment