| Kamanda Mwaruanda |
MWANAMKE mmoja Clemencia Nowa (50) anashikiliwa na polisi
baada ya kumpiga kichwa mume wake na kumsababishia
umauti. wanandoa hao ni wakazi wa kijijini cha Miangalua wilayani
Sumbawanga koani Rukwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa , Jacob Mwaruanda alimtaja
mume aliyekufa kuwa ni Stephen Shauri (72) na kusema mkasa huo ulitokea
alfajiri ya Februari 04, mwaka huu nyumbani kwao.
Akisimulia mkasa huo , Mwaruanda alieleza kuwa mara kwa mara majirani walimsikia akimshutumu mume kuisaliti ndoa yao lakini mume amekuwa akikana kutokuwa na mwanamke mwingine nje ya ndoa yao .
Inadaiwa asubuhi hiyo Clemencia alimkwida mumewe na kumtandika kichwa cha nguvu kilichosababisha aanguke na kufa papo hapo .
Kwamujibu wa Kamanda Mwaruanda mtuhumiwa huyo alikamatwa namajirani zake ambao walimfikisha katika Kituo cha Polisi Laela .
Source:Mchangiaji Rukwa Akisimulia mkasa huo , Mwaruanda alieleza kuwa mara kwa mara majirani walimsikia akimshutumu mume kuisaliti ndoa yao lakini mume amekuwa akikana kutokuwa na mwanamke mwingine nje ya ndoa yao .
Inadaiwa asubuhi hiyo Clemencia alimkwida mumewe na kumtandika kichwa cha nguvu kilichosababisha aanguke na kufa papo hapo .
Kwamujibu wa Kamanda Mwaruanda mtuhumiwa huyo alikamatwa namajirani zake ambao walimfikisha katika Kituo cha Polisi Laela .
إرسال تعليق