JE UNAJUA MADHARA YA KUDANGANYA KWENYE CV YAKO?

Waongo wengi huwa hawakumbuki walichokisema hapo kabla, hivyo huleta uongo mwingine mpya kabisa bila kujua. Hivyo hivyo hutokea pia pale ambapo unaamua kudanganya kwenye CV yako wakati wa kuomba au kutafuta kazi, na wengi wanaona ni kawaida tu ilimradi wapate kazi.

Kumbuka kuwa kazi hiyo inahitaji mtu mwenye vigezo husika, hivyo unapodanganya kwamba una taaluma fulani au ujuzi fulani ambao moja kwa moja haupo kwenye vyeti vyako au kwenye vitu ulivyojifunza itakupa shida kama ni kitu ambacho mwajiri anakuajiri ili atumie ujuzi huo.
Watu wengi hudanganya kwenye ujuzi wao na uwezo wao wa kiutendaji Inawezekana una vyeti stahiki kabisa na unaweza kupata kazi hiyo bali kama unafanyiwa usaili usiongee vitu ambavyo huwezi kuvifanya kwani baadaye utawajibika katika hivyo. Kuna watu wengi hujikuta wanalazimika kuachia ngazi kwa sababu walidanganya kwenye CV zao na hivyo kujikuta hawawezi kazi, hivyo inawabidi waacha kazi kwa visingizio tofauti tofauti.
Ikigundulika umedanganya waajiri wengi hawataweza kukupa kazi kama umepitia kwa taasisi zinazoajiri kwa niaba ya makampuni husika, kwani CV yako na jina lako wataambiana kwenye taasisi hizo. Utasota kutafuta kazi kwasababu ya ujinga wako. Unatakiwa uwe mkweli na ujue nini unafanya kila wakati na kwa kila sehemu unayoomba kazi.


Kama umedanganya kwenye CV yako inamaanisha hata kazini utakuwa mdanganyifu na hilo likigundulika,hautakuwa mtu wa kuaminiwa na mwajiri hivyo kosa dogo la uaminifu litakusababishia kufukuzwa kazi.
Maamuzi ni yako hivyo chukua maamuzi madhubuti kuhakikisha kile unachoandika kwenye CV yako ni ukweli kuhusu wewe na ni kile unachoweza kukifanya.
Ukigundulika mara nyingi unatakiwa kufukuzwa kazi, kwani wewe ni mtu hatari katika nyanja hiyo, inaweza kusababisha kupewa majukumu ambayo yakahatarisha biashara au kampuni na kusababisha matatizo makubwa hivyo kiuhalisia hauhitajiki hata kidogo. Mahali pengine unaweza kupandishwa kizimbani kwa kosa hilo, hivyo uwe mwangalifu usiingie tamaa harafu ukafanya maamuzi ambayo yatahribu taaluma yako.

Post a Comment

أحدث أقدم