Jose
Mourinho amevunja ukimya wake kwa vyombo vya habari na hapo hapo
akaishambulia Manchester City kwa kukiuka taratibu za manunuzi
(financial fair play rules - FFP).
Mourinho
alikuwa kwenye mgomo baridi wa kuzungumza na vyombo vya habari tangu
lilipotokea sakata la kufungiwa kwa mshambuliaji wake Diego Costa kwa
kumsigina mguuni Emre Can wa Liverpool kwenye mchezo wa nusu fainali ya
Capital One Cup.
Kocha huyo wa Chelsea akapigwa faini na FA kwa shutuma zake zilizopitiliza dhidi ya waamuzi.
Lakini
Ijumaa Mourinho akaibuka na kusema: “Kitu pekee ambacho si kizuri ni
kwamba unachuana na timu ambayo haifuati kanuni za FFP.
“Sidhani kama timu inaweza kuwa bingwa huku ikiwa imeadhibiwa, lakini hilo lilishatokea kabla”.
City
imemsajili Wilfried Bony kwa pauni milioni 28 wakati Chelsea ikitumia
pauni milioni 7 licha ya kumnunua Juan Cuadrado kwa pauni milioni 27.

Post a Comment