Watoto 320 wa familia maskini za wafugaji wapata ufadhili wa elimu hadi sekondari

Watoto 320 kutotka familia maskini za jamii za wafugaji mkoani arusha wamepata  ufadhili wa masomo kuanzia  chekechea hadi sekondari kutoka nchi za ulaya hatua  inayolenga kupunguza matatizo yanayowakabili wananchi  wengi wa jamii  hizo yanayochangiwa na ukosefu wa  elimu. 
Wakizungumza wakati wa uzinduzi wa majengo ya shule ya sekondari ya Olosiva iliyoko wilayani arumeru   wanakosoma watoto hao baadhi ya wafadhili wa watoto hao  kutoka Denmark na Finland wamesema pamoja na hatua hiyo  ushirikiano wa dhati wa kuzisaidia jamii za wafugaji    kielimu unahitajika vinginevyo misaada itaendelea  kutolewa na umaskini utaendelea kuwakabili.
Mratibu wa mfuko wa kuwsaidia watoto hao hapa nchini  Dr.Edwin Falc  amesema kimsingi umaskini unazikabili  jamii za wafugaji haupaswi kuwepo kulingana na  rasilimali zinazowazunguka jambo linaloonyesha wazi   kuwa lipo tatizo lingine linalohitaji kupewa kipaumbelea  ambalo ni elimu.
Mwenyekiti wa kitongoji cha Olosiva Bw,Samson Sabaya   amesema utaratibu wa wahisani hao wa kuwekeza katika  elimu na kupeleka misaada moja  kwa moja  kwa walengwa  unafaa kuigwa na wadau wengine kwani unaepusha tatizo.

Post a Comment

أحدث أقدم