Nyasa. Safari ya mwisho ya mbunge wa Mbinga
Magharibi jana ilihitimishwa saa 9.25 alasiri wakati mwili wake
ulipofunikwa na mfuniko mkubwa wa zege uliobebwa na gari maarufu kwa
jina la “kijiko”.
Haikuwa kitu cha kawaida wakati gari hilo kubwa
likishusha mfuniko huo wa zege kwenye kaburi la mwimbaji huyo maarufu wa
nyimbo za uhamasishaji za CCM na kiongozi wa kundi la Tanzania One
Theatre (TOT), lakini majonzi yaliwafanya waombolezaji kulichukulia
tukio hilo kuwa la kawaida.
Safari ya Komba, iliyoanza miaka 61 iliyopita
kwenye kijiji cha Lituhi ambako aliazikwa jana, ilikamilishwa kwa salamu
mbalimbali ambazo zilielezea ushupavu wa kapteni huyo mstaafu wa jeshi.
Mazishi hayo yaliyohudhuriwa na mamia ya wananchi,
wakiwamo viongozi mbalimbaliwakiongozwa na Rais Jakaya Kikwete na mkewe
Salma, yalifanyika katika makaburi ya Misheni,katika Kijiji cha Lituhi
(Bundi) wilayani Nyasa mkoani Ruvuma.
Nyuso za majonzi zilitawala kwa waombolezaji
waliojitokeza nyumbani kwa marehemu, takriban mita 500 kutoka katika
makaburi hayo na baadaye katika misa iliyofanyika kwenye uwanja wa Shule
ya Msingi ya Lituhi, ikiongozwa na Askofu John Ndimbo wa Jimbo Katoliki
la Mbinga.
Kaimu katibu wa Bunge, John Joel, akisoma wasifu
wa marehemu, alisema Kapteni Komba aliyefariki dunia Februari 28, mwaka
huu akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya TMJ jijini Dar es Salaam,
alikuwa anasumbuliwa na maradhi ya shinikizo la damu na mara kadhaa
Ofisi ya Bunge ilimpeleka India kwa matibabu. Pia alikuwa na tatizo la
kisukari ambalo ndilo lililochukua maisha yake.
Mazishi hayo yalishuhudiwa na viongozi mbalimbali,
akiwamo Edward Lowassa, ambaye alikuwa Waziri Mkuu, Waziri wa Kilimo,
Chakula na Ushirika, Steven Wasira, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu
(Sera, Utaratibu na Bunge), Jenister Mhagama na mbunge wa Songea Mjini,
Dk Emmanuel Nchimbi.
Wengine ni Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete,
Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi, Ali Abdallah Ali, Waziri wa Nchi,
Ofisi ya Rais (Kazi Maalumu), Profesa Mark Mwandosya na Spika wa Bunge,
Anne Makinda.
Uwanja wa ndege
Kwenye Uwanja wa Ndege wa Songea, viongozi
mbalimbali waliwasili kwa ndege za kukodi na Lowassa ndiye aliyefungua
mlango kwa ndege iliyotua saa 2:33 asubuhi akiambatana na mbunge wa
Korogwe Vijijini, Stephen Ngonyani.
Haikupita muda mrefu, ndege nyingine ilitua saa
2:50 ikiwa na Spika Makinda na msafara wake uliomjumuisha mbunge wa
Ludewa, Deo Filikunjombe.
Saa 3:22 ilitua ndege iliyobeba ujumbe wa CCM
ukiongozwa na Kinana. Wengine waliokuwamo ni naibu katibu mkuu ambaye
pia ni Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba, katibu wa itikadi na
uenezi, Nape Nnauye na mwimbaji wa kikundi cha TOT, Khadija Kopa. Pia
baadaye Rais Kikwete alitua na ndege ya Serikali

إرسال تعليق