Linex na wimbo mpya, Lina na dili jipya na muigizaji Aunty Ezekiel ishu ya kujifungua #255


Kwenye zile info zilizosikika leo kwenye 255, msanii Linex amezungumzia wimbo wake mpya wa salima aliomshirikisha Diamond Platimuz aliouachia leo, amesema leo anasambaza wimbo huo kwenye vituo mbalimbali vya Radio na Television na yuko kwenye mikakati ya kuipeleka kwenye vituo vikubwa vya Television nje ya nchi, ambapo Audio ya wimbo huo imefanywa na producer Tuddy Thomas huku video ikifanywa na director mkali Bongo Adam Juma.
DSC_0092 
Msanii Lina amezungumzia tukio alilolifanya leo la kusaini dili la kuwa Balozi wa kinywaji kipya cha Jebel dili alilopata kutokana na ushawishi mkubwa alionao kwa watu  ambalo atafanya kwa mwaka mzima, ukiwa ni mkataba wake wa tatu kwani alishaingia mikataba mingine miwili ya kuwa Balozi wa vitu tofauti na inamsaidi kupata fedha za kujiendeleza kwenye mziki.
Aunt-Ezekiel-222 
Story ya mwisho kwenye 255 inahusu video aliyoposta muigizaji Aunty Ezekiel kwenye ukurasa wake wa Istagram jana usiku ,ikimuonyesha akiwa Hospitali na watu wakaanza kumpongeza kwa kujifungua, baada ya siku yake kutokuwa hewani 255 iliamua kumtafuta Mose Iyobo anaesemekana kuwa baba wa mtoto huyo, ambae amesema kuwa alikuwa anashoot video ya movie mpya aliyocheza na msanii Dude.
Ili kuweza kusikiliza story zote za 255 bonyeza play hapa chini…

Post a Comment

Previous Post Next Post