Rais
Jakaya Kikwete amemtumia salamu za rambirambi mkuu wa mkoa wa Iringa,
Amina Masenza kufuatia ajali mbaya ya barabarani iliyotokea Mafinga
katika mkoa wa Iringa eneo lijulikanalo kwa jina la Changarawe, ambayo
imepoteza uhai wa watu zaidi ya 40 waliokuwa wakisafiri kwa basi hilo na
wengine kadhaa kujeruhiwa.
Katika
salamu zake hizo, rais Kikwete amewahakikishia wafiwa wote kuwa yuko
pamoja nao katika kuomboleza msiba wa ndugu na jamaa zao na kuwaombea
kwa mwenyezi mungu, mwingi wa rehema watu wote waliojeruhiwa kwenye
ajali hiyo wapone haraka, ili waweze kuungana tena na ndugu na jamaa
zao.
Post a Comment