WANAJESHI wawili waliohukumiwa kunyongwa hadi kufa baada ya 
kupatikana na hatia ya kumuua Swetu Fundikira ambaye ni mtoto wa ndugu 
wa marehemu Chifu Abdallah Fundikira, wamekata rufaa kupinga adhabu 
hiyo.
 
Wanajeshi hao ambao ni ndugu , MT 75854 Koplo Ally Ngumbe wa Jeshi la
 Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) Kikosi cha Kunduchi na MT 85067 
Koplo Mohamed Rashid (JKT Mbweni), wamewasilisha rufaa hiyo katika 
Mahakama ya Rufani.
Katika rufaa yao, wanajeshi hao wana hoja tatu wakipinga hukumu ya 
kunyongwa hadi kufa iliyotolewa Novemba 20, 2012 na Jaji Zainab Mruke wa
 Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam.
Katika hoja zao, wanajeshi hao wanadai Jaji alikosea kisheria kutoa 
uamuzi kwa kutozingatia kanuni za kuthibitisha mashitaka pasipo kuacha 
shaka yoyote, ambalo ni jukumu la upande wa mashitaka.
Aidha, wanadai Jaji alikosea kisheria kwa kutoa hukumu inayoegemea 
ushahidi wa kimazingira, bila kuzingatia ushahidi wa utetezi wa wakata 
rufaa. Katika hoja nyingine wanadai alishindwa kuchanganua itirafu 
katika majina kwenye taarifa ya uchunguzi wa chanzo cha kifo.
Awali, wakati hukumu hiyo inatolewa walihukumiwa washtakiwa watatu 
akiwemo aliyekuwa MT 1900 Sajenti Roda Robert wa Jeshi la Kujenga Taifa 
(JKT) Kikosi cha Mbweni, ambaye alifariki dunia mwaka jana mkoani Dodoma
 wakati akisubiri utekelezwaji wa hukumu hiyo.
Katika hukumu hiyo, Jaji Zainab alisema upande wa mashitaka 
umethibitisha kesi yao bila shaka na hivyo Mahakama imeona kuwa 
washitakiwa wote wana hatia na walimuua marehemu Fundikira kwa 
kukusudia.
Hata hivyo, alisema hakuna shahidi aliyethibitisha kuwa aliwaona 
washitakiwa wanavyomuua Swetu, bali mashahidi watatu walithibitisha 
kuwaona washtakiwa wakiwa na Swetu kabla ya kukutwa na mauti.
Alisema anawatia hatiani washtakiwa na kuwahukumu kunyongwa hadi kufa
 kwa kuwa ushahidi wa mazingira umeowanyooshea kidole washitakiwa kuwa 
wanahusika na mauaji hayo.
Ilidaiwa Januari 23 ,2010 katika eneo la Kinondoni, Dar es Salaam, washtakiwa hao walidaiwa kumuua marehemu Fundikira

Post a Comment