KUNGURU: NIMETUMWA SANA POMBE BONGO MOVIE

IMELDA MTEMA
MSANII wa sinema za Kibongo, Brenda Malembeka ‘Kunguru’ ameibuka na kuanika ukweli wa maisha yake kuwa kabla ya kutoka kisanaa, aliteseka sana kwa kutumwa pombe na wasanii waliokuwa tayari na majina makubwa.
Msanii wa sinema za Kibongo, Brenda Malembeka ‘Kunguru’.
Akizungumza na mwanahabari wetu, Kunguru alisema kwa kipindi hicho ilimlazimu akubali kutumwa pombe na mastaa kwani lengo lake lilikuwa ni kupatiwa nafasi ya kucheza uhusika ukuu. “Nilikubali sana kutumwa pombe na mastaa wakubwa ili lengo langu litimie, nashukuru Mungu kwa sasa nimepata shavu kwenye filamu inaitwa Asante iliyoandaliwa na Masai Media Group,” alisema Kunguru.

Post a Comment

أحدث أقدم