MAMA AJIFUNGUA MAPACHA WANNE KWA MKUPUO MKOANI KIGOMA, AOMBA MSAADA KWA WATANZANIA


Na Editha Karlo, Globu ya Jamii - Kigoma

MKAZI wa Kijiji cha Buzebazeba katika Manispaa ya Kigoma Ujiji, Zuwena Abdu (29) jana amejifungua watoto mapacha wanne kwa mkupuo katika Hospital ya Mkoa  wa Kigoma (Maweni).

Zuwena alisema kuwa watoto aliojifungua wenye jinsi ya kiume ni  watatu na  mmoja ambaye ni wa mwisho ana jinsi ya kike ,wa kwanza akiwa na uzito wa kilo 1.8,pili 2.5 wa tatu 1.7 na wanne 1.7.

Alisema watoto hao alijifungua jana majira ya saa kumi na mbili jioni salama  kwa njia ya kawaida 

Zuwena alisema huo ni uzazi wake wa tano ambao awali alijifungua wanne kwa njia ya kawaida kwahiyo jumla anaidadi ya watoto nane.

''Kwanza nina mshukuru mungu kwa kuniwezesha kujifungua salama watoto wote na wakiwa hai kutokana na hali duni ya  kiuchumi ya familia yetu mimi na mume wangu tunaomba Watanzania wenye mapenzi mema watusaidie ili tuweze kuwalea hawa watoto,mume wangu hana kazi na mimi sina kazi''alisema mama huyo

Muuguzi wa zamu katika wodi  ya wazazi  Agness Nguvumali alisema kuwa alifikishwa mama huyo alifikishwa hospitalini hapo siku ya jumatatu saa kumi jioni akiwa na uchungu na ilipofika saa kumi na mbili akawa amejifungua mapacha wanne kwa njia ya kawaida salama.

Muuguzi huyo alisema kuwa watoto wote wana afya njema alisema wataendelea kubaki hospitalini hapo kwaajili ya uangalizi wa karibu wa madaktari.

Agness amewaomba Watanzania,mashirika mbalimbali kujitokeza kumsaidia mama huyo ili aweze kuhudumia watoto wake hao kwakuwa hali yake ya uchumi na mume wake siyo nzuri na utunzaji wa mapacha hao unahitaji uwezo wa nguvu ya ziada.

 YEYOTE MWENYE MSAADA KWA WATOTO HAO ANAWEZA KUWASILIANA KWA KUTUMIA NAMBA 0752202783


Mama wa watoto mapacha wanne, Bi. Zuwena Abdu akiwa wodini baada ya kujifungua.

Muuguzi wa zamu katika Wodi ya wazazi ya Hospital ya Mkoa wa Kigoma (Maweni), Agness Nguvumali akiwaangalia mapacha wanne waliozaliwa hospitalini hapo.

Post a Comment

Previous Post Next Post