VAN GAAL AONYA: MANCHESTER UNITED BADO IKO KWENYE MBIO ZA UBINGWA

Kocha wa Manchester United Louis van Gaal ameonya kuwa timu yake bado iko kwenye mbio za ubingwa licha ya kuwa nyuma kwa pointi nane dhidi ya vinara wa Ligi Kuu Chelsea.
Van Gaal pia amekiri kuwa Marouane Fellaini amekuwa nguzo muhimu kutokana na kuimarika kwa kiwango chake.
Ushindi dhidi ya Aston Villa Jumamosi utaongeza presha kwa majirani zao Manchester City ambao hawatacheza hadi Jumatatu pale watakapoikabili Crystal Palace.
Van Gaal ambaye amethibitisha kuwa Robin van Persie bado ni majeruhi, amesema bado kuna vita vya kugombea nafasi ya nne lakini lolote linaweza kutokea hata kwenye kuwania taji.

Post a Comment

أحدث أقدم