Wachezaji wa Yanga.
YANGA imekanyaga ardhi ya
Zimbabwe na kuitikisa kwa kuwa kila kona ya Mji wa Bulawayo
wanaizungumzia mechi yao ya Kombe la Shirikisho dhidi ya FC Platinum.
Yanga wametua huku wakionyesha wao ni wazoefu wa michuano wa
kimataifa na wana akili nyingi ya kung’amua mambo kadhaa ambayo
waliwekewa kama mtego na wapinzani wao FC Platinum waliowabutua kwa
mabao 5-1 jijini Dar.
FC Platinum wanahaha kila sehemu kabla ya mechi ya leo itakayopigwa
katika mji wa madini wa Zvishavane ambao uko takribani Kilomita 200
kutoka hapa Bulawayo.Yanga walitua hapa saa tisa jioni na ndege
inayomilikiwa na Serikali ya Tanzania na kupokelewa na mashabiki
waliotangulia hapa wakiwa wanaongozwa na Katibu wa Baraza la Wazee
Yanga, Mzee Ibrahim Akilimali na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano, Jerry
Muro.
Mara baada ya kutoka nje ya uwanja, walipitiliza moja kwa moja hadi
katika basi lililowaleta mashabiki kutoka jijini Dar na kuacha mabasi
mawili yaliyokuwa uwanjani pale.Angalia walichokifanya Yanga. Wakati FC
Platinum walileta basi lao, Yanga walileta basi jingine walilolikodi na
kulilinda kwa siku kadhaa kwa kuwa ndiyo wangetumia wachezaji.
Lakini baada ya kufika, mabasi yote mawili wakaachana nayo na kupanda
lile la mashabiki huku mashabiki wakipanda la wachezaji.Mzee Akilimali
naye akatoa mpya baada ya kuanza kumwaga maji ‘fulani’ katika eneo la
basi wanalopanda wachezaji, mwisho akawazuia kutoa mikono yao kwa mtu
yeyote yule.
Ukiachana na basi, Yanga walikataa chakula kilichopikwa katika hoteli
ya nyota tano ya Holiday Inn iliyo mjini hapa na kwenda kula kile
maalum kilichopikwa na Watanzania.FC Platinum hawakuchoka, waliendelea
kufanya ushushu kwa kutuma watu waliofika uwanja wa ndege na kujaribu
kufanya uchunguzi lakini hawakuambulia kitu.
Hasira zao zikaishia kwa waandishi wa habari, wakitaka kuwajua ili
wawaondoe na ikiwezekana kuwarudisha Tanzania, lakini umafia mwingine
ukafanyika kwa kuwavisha jezi za Yanga kuonyesha kuwa ni mashabiki.
Juhudi za FC Platinum kutaka kulipa kisasi cha kutundikwa mabao 5-1 zimekuwa kubwa, lakini wanaonekana kupania kuanza kuucheza mpira nje ya uwanja.
Juhudi za FC Platinum kutaka kulipa kisasi cha kutundikwa mabao 5-1 zimekuwa kubwa, lakini wanaonekana kupania kuanza kuucheza mpira nje ya uwanja.
Post a Comment