Kuna msanii kutoka KENYA amezuiliwa kuachia video yake mpya, kisa hiki hapa

11252608_1402222130104371_1369530340_n
Leo asubuhi msanii kutoka Nairobi Kenya anajulikana kwa jina la COLONEL MUSTAFA alinitumia ujumbe mfupi kupitia WhatsApp yangu na kuniambia niwajulishe mashabiki wake wote kuhusu kuhairishwa kwa video yake mpya ya DODOMA SINGIDA.

“Ningependa kujulisha mashabiki wangu kuwa video yA DODOMA SINGIDA ambayo ilifaa kutoka jana tarehe 22/5/2015 itachelewa kidogo kutoka, kutokana na jana mimi kushikwa na police (CID) kwa makosa ambayo nadaiwa kuwa nilitumia model ambaye ni mke wa mtu mashuhuri nchini Kenya bila mumewe kujulishwa kabla ya shooting..kuna madaliko lazima yafanyike ndio video ya dodoma singida iweze kutoka..Asante na nina wapenda wote”

11283317_1604866986438788_1765257322_n

Post a Comment

Previous Post Next Post