WATU 6 WAJERUHIWA BAADA YA BOMU KURUSHWA KWA MKONO WAKATI WAKITOKA KWENYE MAADHIMISHO YA MEI MOSI

Hofu ya ugaidi  imezidi kutanda katika wilaya ya kilombero  baada ya watu  sita  kujeruhiwa vibaya na bomu lililorushwa kwa mkono  wakati wakitoka katika  maadhimisho ya mei mosi  katika kijiji cha msolwa ujamaa kata ya sanje  wilayani kilombero mkoani Morogoro .
Katika hospitali ya ST KIZITO MIKUMI  walikolazwa majeruhi wa tukio hilo  wamesema  bomu hilo lilirushwa na vijana wawili   baada ya kutiliwa shaka na wananchi wa kijiji cha msolwa ujamaa kata ya sanje tarafa ya mangula kuwaweka chini ya ulinzi kwa ajili ya kuwapekua ambapo  vijana hao walirusha  bomu  na kujeruhi wananchi pamoja na baadhi ya viongozi wa serikali waliokuwa kwenye gari ya mweneyekiti wa halmashauri wakitokea katika maadhimisho ya mei mosi ambapo  wameomba jeshi  la polsi kufanya uchunguz kufuatia matukio  yanayoashiria ugaidi kuendelea kuandama wakazi  wa kilombero.
 Nao viongozi wa kata akiwemo diwani wa kata ya sanje David Ligazio wamesema ipo haja ya serikali kuongeza nguvu ya jeshi la polisi ikiwa ni pamoja na magari ya usafiri na kutafuta vifaa vinavyo weza kuchunguza maeneo ya milima ya udizungwa na Ruaha   ambapo wamebaini  wahalifu wengi  wamewaona wakitokea katika misitu hiyo  mara kw amara.
Kamanda wa polisi mkoa wa morogoro Lenard Pual  amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo ambapo amesema hadi sasa jeshi la polisi linawatafuta watuhumiwa  hao ambao baada ya kurusha bomu hilo limejeruhi dereva wa  mweneyekiti wa halmashauri ya wilaya ya kilombero  na kuharibu gari ya halmshauri pamoja na wananchi wa kijiji cha msolwa ujamaa.
Tukio hilo limetokea ndani ya siku 14 baada ya watuhumiwa  9 kukamatwa msikitini wakiwa na milipuko 30, sare za jeshi, bendera nyeusi pamoja na vitu mbalimbali vya kufanyia uhalifu huku mmoja akichomwa moto na wananchi wenye hasira akiwa katika harakati za kutoroka baada ya kumchoma askari kwa jambia shingoni katika   tarafa ya kidadu wilayani kilombero.
ITV

Post a Comment

أحدث أقدم