Inatia huruma, sehemu ya haja kubwa ya Mtoto Yathib Rajab.
Boniphace Ngumije na Chande Abdallah
MASKINI mtoto huyu!
Unapojaliwa kupata mtoto akiwa mzima asilimia 100 unatakiwa kumshukuru
Mungu. Mwajuma Juma (25) mkazi wa Mbagala, Sabasaba Dar es Salaam,
ameingia kwenye mtihani mzito tangu ajifungue mwanaye Yathib Rajab mwaka
mmoja uliopita, akiwa hana sehemu ya kujisaidia haja kubwa.
Mwajuma Juma akiwa na mwanaye Yathib Rajab.
Baada ya kugundulika kuwa na tatizo hilo
madaktari wa Hospitali ya Taifa Muhimbili walimfanyia opasuaji na
kumtoboa kwenye tumbo lake upande wa kulia na kuchomoa sehemu ya utumbo
ambayo imekuwa ikitumika kumsaidia mtoto huyo kujisaidia.
Mwajuma Juma akimbembeleza mwanaye Yathib Rajab..
Akizungumza na Ijumaa
juzi, Mwajuma alisema kuwa madaktari walimwambia kuwa Aprili mwaka huu
alitakiwa kurudi hospitalini hapo ili wamfanyie upasuaji wa
kumtengenezea sehemu ya kutolea haja kubwa.
“Madaktari waliniambia utaratibu wa
kuwasaidia bure watoto wenye tatizo hili umesogezwa mbele mpaka mwaka
2019. Ili sasa afanyiwe upasuaji zinahitajika shilingi 1,350,000 ambazo
sina kwani baba wa mtoto huyo alifariki dunia wakati nina mimba ya miezi
sita.
Naomba msaada kwa Watanzania wenzangu ili mwanangu afanyiwe upasuaji, anateseka sana,” alisema mama huyo.
Yeyote aliyeguswa na tatizo la mtoto huyu anaweza kutuma chochote au kuwasiliana na mama yake kwa namba 0652 082 464.
Post a Comment