Msanii wa filamu Bongo, Fatuma Ayubu `Bozi’ akihamisha vitu vyake.
Mayasa Mariwata na Gladness Mallya
MAJANGA! Msanii wa
filamu Bongo, Fatuma Ayubu `Bozi’ amejikuta akifungasha virago na kuhama
kwenye nyumba aliyokuwa akiishi maeneo ya Kinondoni jijini Dar kutokana
na mjengo huo kutawaliwa na mauzauza yanayosadikiwa kuwa ya
kishirikina.
….Akiendelea kutoa vitu vyake.
Chanzo makini kilicho jirani na nyumba
aliyokuwa akiishi mwanadada huyo kilieleza kuwa, baada ya kuvumilia
vimbwanga vya kishirikina ameamua kuondoka.
“Hii
nyumba wapangaji huwa hawadumu kwa kushindwa kustahimili wanayoyaona
sijui ina balaa gani, tunashangaa yeye ameweza kukaa kwa mwaka mzima na
kuvumilia majanga yote, inataka moyo.
“Sasa
leo uzalendo umemshinda baada ya mpangaji mwenziye kufariki ghafla wiki
iliyopita, ambapo siku moja kabla ya kifo chake alipambana na paka
aliyekojoa mlangoni, tangu itokee hiyo ishu amekuwa akija hapo
kuchungulia nyumba na kuondoka, leo kaona isiwe tabu, anahamisha vitu
vyake,” kilisema chanzo.
Baada
ya kupata fununu hizo bila kupoteza muda wadakuzi wetu waliibuka
nyumbani kwa msanii huyo na kumkuta akiwa kwenye hekaheka ya kuhama na
kukiri kuwa amelazimika kufanya hivyo kutokana na aliyokuwa akiyaona
kwenye nyumba hiyo.
Fatuma Ayubu `Bozi’ katika pozi.
“Kuna muda nikiwa chumbani nasikia taa
zinawashwa na kuzimwa nikitazama sioni mtu, wakati mwingine paka anakuja
chumbani na kucheza kwenye kioo ukimfukuza na kufunga mlango dakika
chache unamuona tena na cha kustaajabisha nakuwa najiuliza amepita wapi
sipati jibu, kwa ujumla nyumba hii ina mauzauza kibao ambayo nimeshindwa
kuyavumilia, hali ni mbaya nahamia kwa rafiki yangu,” alisema Bozi.
Post a Comment