Mh. Majaliwa amwagiza mkurugenzi kuwajengea vyoo wanafunzi wa kike wa Kihadzabe


SAM_2825
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (OWM) – TAMISEMI (Elimu), Mhe. Kassim Majaliwa (MB) (aliyevaa miwani) akisalimiana na viongozi pamoja na wazazi wa wanafunzi wa shule ya msingi Munguli, kata ya Mwangeza,tarafa ya Kiru mi, wilayani Mkalama wakati wa ziara ya siku moja wilayani humo kutembelea maeneo ya wanayoishi wanafunzi wa jaamii ya kabila la Wahaadzabe.
SAM_2826
Wanafunzi wa shule ya msingi Munguli wakiimba wimbo wa shule yao wakati wakimpokea Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (OWM) – TAMISEMI (Elimu), Mhe. Kassim Majaliwa (MB) alipowatembelea shuleni kwao.
SAM_2836
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (OWM) – TAMISEMI (Elimu), Mhe. Kassim Majaliwa (MB) akiongeaa na wazazi pamoja na walezi wa  wanafunzi wa shule ya msingi Munguli.
SAM_2835
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (OWM) – TAMISEMI (Elimu), Mhe. Kassim Majaliwa (MB) (wa kwanza kutoka kushoto) akisikiliza maoni, ushauri pamoja na maswali kutoka kwa wazazi wa wanafunzi wa shule hiyo.
SAM_2829
Baadhi ya wazazi wa wanafunzi wa jamii ya kabila la wahadzabe wakimsikiliwa Mh. Majaliwa alipokuwa akaiongea nao kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya shule hiyo.
SAM_2831
Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Mkalama pamoja na baadhi ya wanafunzi wa shule ya msingi Munguli (waliovaa sare za shule).
SAM_2832
Baadhi ya watumishi wa Halmashauri ya wilaya ya Mkalama pamoja na wazazi wa wanafunzi wa shule ya Msingi Munguli wakimsikiliza Mh. Kassimu Majaliwa (hayupo pichani).
Na Jumbe Ismailly,Mkalama           
NAIBU Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (OWM) – TAMISEMI (Elimu), Mhe. Kassim Majaliwa (MB) amemwagiza Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Mkalama kuhakikisha anawajengea matundu ya vyoo wanafunzi wa jamii ya kabila la wahadzabe wa kike wa shule ya msingi Munguli ili nao waweze kupata sehemu ya kujisaidia kwa nafasi badala ya ilivyo sasa ambapo wanachangia na wavulana.
Naibu waziri huyo, Kassimu Majaliwa alitoa agizo hilo alipokuwa akiongea na wazazi na wanafunzi wa shule ya msingi Munguli,iliyopo katika Kata ya Mwangeza,tarafa ya Kirumi kufuatia taarifa ya mkurugenzi huyo kwamba wanafunzi wa kike na wale wa kiume wanachangia matundu ya vyoo.
“Na leo nimemwambia mkurugenzi kati ya bweni na bweni kuna choo pale cha matundu mawili,ananiambia huku wavulana na kule wasichana,haiwezekani,tuamue tu lile jengo liwe la wavulana peke yao au wasichana peke yao’alibainisha naibu waziri huyo.
Alisema Majaliwa kwamba ni vyema wasichana wakajengewa matundu ya vyoo eneo mbali na wavulana ili kuwaepusha kukutana na wavulana hususani nyakati za usiku,kwani endapo utaratibu ulipo sasa utaendelea utahatarisha maisha ya wanafunzi hao wa kike watakapokuwa wakikutana usiku na wavulana chooni.
Hata hivyo Majaliwa hakusita kujizuia furaha yake kutokana na kitendo kilichofanywa na mkuu wa mkoa wa Singida,Dk.Parseko Kone cha kuifufua shule hiyo iliyojengwa katika kipindi cha utawala wa baba wa taifa,marehemu Julius Kambarage Nyerere,iliyokuwa imeanza kupoteza umaarufu wake.
Naye afisa elimu wa Halmashauri ya wilaya ya Mkalama,Mwisungi Kigosi alielezea changamoto zinazoikabili shule ya msingi Munguli kuwa ni pamoja na upungufu wa matundu ya vyoo vya wanafunzi,madawati,meza,viti,kabati,uhaba wa maji,chakula,mafuta ya kupikia,chumvi,sabuni na nguo za kubadilisha wanafunzi wa bweni.
Hata hivyo licha ya kuwepo kwa changamoto hizo,afisa huyo mwenye dhamana ya kusimamia sekta ya elimu alibainisha utatuzi wa changamoto hizo kuwa ni Miss Tanzania namba tatu ambaye pia ni Miss Singida namba moja Miss kanda ya kati, Dorice Mollel ametoa msaada wa mablanketi 40 pamoja na vitabu.
Aidha Kigosi alisema pamoja na Miss Singida huyo kutoa msaada huo,vile vile aliahidi kutafuta wadau wa maendeleo kujenga maktaba ya kisasa itakayotumika kwa ajili ya wanafunzi hao.
Kwa upande wao baadhi ya wazazi na walezi wa wanafunzi hao,mwenyekiti wa jamii ya kabila la wahadzabe,Edward Mashimba alielezea kero zinazowakabili wananchi wa eneo hilo kuwa ni pamoja na ubovu wa barabara,mawasiliano ya simu na uvamizi katika hifadhi ya msitu waliokuwa wakiutegemea kujipatia chakula.
Wilaya ya Mkalama ina jumla ya vituo vitatu vya elimu nje ya mfumo rasmi (MEMKWA) katika shule za msingi Mwanga,Nkungi na Chemchemu huku ikiwa na shule binafsi moja inayomilikiwa na shirika la Dini la Roman Catholic yenye jumla ya wanafunzi 189,ambao kati yao wavulana ni 84 na wasichana ni 105.

Post a Comment

Previous Post Next Post