CHADEMAWATIA AIBU..!! WAKAMATWA NA MASHINE YA BVR WAKIANDIKISHA WATU USIKU NA KUWALIPA HUKO WILAYANI KAHAMA

Jeshi la polisi wilayani kahama mkoani Shinyanga limekamata mashine moja ya BVR ikitumika kuandikisha wapiga kura saa tatu usiku nyumbani kwa mwenyekiti wa mtaa wa Nyakato wilayani humo Mayunga Alphonce kupitia CHEDEMA, huku wakiwalipa shilingi 5,000 kila mmoja. 

Akizungumza leo na waandishi wa Habari mkuu wa wilaya ya kahama Benson Mpesya amesema tukio hilo limetokea jana majira ya saa 3 usiku katika mtaa wa nyakato ambapo mashine hiyo ilikutwa ikiwa inafanya kazi ya kuandikisha wapiga kura.

Mpesya amesema kuwa vyombo vya usalama wilayani humo vilipata taarifa kutoka kwa raia wema ambazo zimewezesha kukamatwa kwa mashine hiyo pamoja na vitambulisho vitano ambavyo tayari vilikuwa vimeshakamilika kuandikishwa.

Ameongeza katika harakati za kukamata mashine hiyo pia wameweza kumkamata mhamiaji haramu mmoja raia wa Burundi ambaye tayari alikuwa ameshaandikishwa na mashine hiyo akiwa ndani ya nyumba ya mwenyekiti huyo wa mtaa.

Mpesya amesema jeshi la Polisi wilayani humo linamshikilia kaimu afisa mtendaji wa kata ya Nyasubi Lugina Misango ambaye ndiye mwenye dhamana ya kusimamia mashine hizo kwa kosa la kuruhusu mashine hiyo kutumika nyumbani kwa myekiti wa mtaa.

Katika hatua nyingine Mpesya amewataka waandishi wa habari wanaotumiwa kukanusha taarifa hiyo, kutambua kuwa ofisi yake ni mamlaka kamili ya serikali na kwamba wasubiri hatua za kisheria kwani ushahidi wa kukamatwa kwa mashine hiyo upo kituo cha polisi.
Tangu kuanza kwa zoezi la uandikishaji wapiga kura katika daftari la kudumu la wapiga kura wilayani humo hilo ndio tukio la kwanza la aina yake ambalo limevuta hisia, na Mpesya amesema jeshi la polisi bado linaendelea na uchunguzi.

Post a Comment

Previous Post Next Post