Kha! Diamond hii sasa sifa

KWELI wa mbili havai moja. Nyota ya msanii wa muziki wa kizazi kipya nchini, Diamond Platnumz, inazidi kung’aa baada ya juzi Jumamosi kushinda tuzo nyingine ya kimataifa, ikiwa ni wiki moja tu tangu anyakue tuzo ya MTV MAMA 2015.
Staa huyo wa ‘Mdogo Mdogo’ na ‘Number One’ alinyakua tuzo hiyo katika tuzo za Africans Achievers Awards 2015 zilizofanyika Afrika Kusini.
Ushindi huo umezidi kumfanya Diamond kuzidi kutusua na kuwafunga mdomo wale wote wanaombeza na wasiomkubali kwa mafanikio aliyonayo katika anga la kimataifa.
Diamond aliandika kwenye akaunti yake ya Instagram kuonyesha furaha yake na kumshukuru Mungu kwa ushindi huo ambao umezidi kumweka matawi ya juu.
“Thanks God gof Keep Blessing my Hustle....African Artiste of the Year#AfricansAchievers Awards 2015.” Ujumbe huo ulisomeka hivyo na kuendeelea;
“Shukrani nyingi ziwafikie uongozi wangu kwa kuhakikisha unanisimamia ipasavyo. Mama Yangu kipenzi Sandrag. My Beautiful Baby@Zarithebosslady. Media zote na mashabiki zangu pendwa kwa kuendelea kunisapot bega kwa bega,” alimalizia Diamond katika ujumbe wake huo.
Wakati akisherehekea mafanikio tayari mkali huyo tayari yupo kwenye kinyang’anyiro kingine cha kuwania tuzo za AFRIMMA 2015 zinazotarajiwa kutolewa hivi karibuni huko Nigeria

Post a Comment

Previous Post Next Post