Kidoti, Kuambiana wafunika ZIFF 2015

TAMASHA la Kimataifa la Filamu la Zanzibar (ZIFF) 2015 limefungwa rasmi juzi Jumamosi katika Ngome Kongwe, Zanzibar na kushuhudiwa aliyekuwa nyota wa filamu nchini, Adam Kuambiana ambaye ni marehemu kwa sasa na mwanadada Jokate Mwegelo ‘Kidoti’ wakifunika mbaya.
Kwa jumla tamasha la mwaka huu lilifana vilivyo kwa burudani iliyotolewa na wasanii mbalimbali wa ndani na nje ya nchi walioshirikishwa na washindi mbalimbali walitwaa tuzo zilizotolewa kwa msimu wa mwaka 2014-2015.
Kwa upande wa Tanzania, baadhi ya filamu zake zilifanya vyema kwa kunyakua tuzo kadhaa huku wasanii wake nao wakifanya yao, ikiwamo kushuhudia marehemu Kuambiana akiibuka kuwa Mwigizaji Bora wa Kiume wa Ziff 2015.
Kuambiana aliyefariki Mei mwaka jana na Kidoti kila moja alinyakua tuzo ya Mwigizaji Bora kwa msimu wa mwaka 2014/2015.
Kadhalika filamu mbili za Kibongo zilitusua kimtindo katika tamasha hilo kwa kunyakua tuzo zikipenya kwenye rundo la filamu karibu 500 zilizoshiriki kinyang’anyiro hicho kwa mwaka huu.
Filamu hizo ni ‘Mr Kadamanja’ iliyoongozwa na kuigizwa na marehemu Kuambiana ambayo ndiyo pia iliyompa tuzo aliyonyakua na nyingine ni Daddy’s Wedding iliyonyakua tuzo mbili.
Tuzo ya kwanza kwa filamu hiyo ile ya Chaguo la Watu (People’s Choice Award), pia kutoa Mwigizaji bora ambaye ni marehemu Kuambiana, wakati Daddy’s Wedding ilinyakua tuzo ya ‘Best Cinematography’ na ile ya Director Bora ambayo ilikwenda kwa Honeymoon Mohamed.https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEggJ2lKSbnDHa7wRz3YSyOibgwFwXpYCmo7fgZM6dVpNQPk94minnIBsV5XNdSRHVTiegnUXp3RrCwHxkvzOpL3on4gE-t2HqGxDwbi8QwcKolzH5kZ-EV8HWZLDoWdTiPaCOz9Irp77P1f/s1600/ZIFF+NEW.JPG
Mrembo Jokate Mwegelo yeye alinyakua tuzo ya Mwigizaji Bora wa Kike kupitia filamu ya ‘Mikono Salama’ iliyoandaliwa na Jacob Steven JB.
Jokate aliandika kwenye mtandao wake kushukuru kwa ushindi huo na kuelezea ni moja ya mafanikio aliyokuwa akiyaota na kuwashukuru wote waliompa sapoti katika sanaa yake.
Nayo filamu ya ‘Samaki Mchangani’ ilishinda tuzo za Best Film in Sound, huku tuzo ya Zuku Best Feature Film ikishinda filamu ya ‘Kutakapokucha’.
Katika upande wa European African Film Festival Awards, tuzo ya Best African Film ilikwenda kwa WAZI? FM – Dir: Faras Cavallo.
Filamu bora za ukanda wa Afrika Mashariki EAC-EAFN zilizotwaa tuzo usiku wa kuamkia jana ni pamoja na ‘Going Bongo’ ambayo imetayarishwa na Dean Matthew Ronalds iliyokuwa filamu bora ya mwaka kutoka Afrika Mashariki

Post a Comment

Previous Post Next Post