
UNAWEZA PITIA:- MAISHA TANZANIA <= Kwa kubofya hapo
Lakini si hivyo tu, Azam haikutaka kukutana na
Yanga kwenye michuano hiyo kwenye hatua ya mtoano. Kocha wa Azam,
Stewart Hall alisema: “Unapocheza na Yanga unacheza dhidi ya mashabiki
zaidi ya 45,000 na pia waamuzi na baadhi ya maofisa, hiyo inaufanya
mchezo kuwa mgumu zaidi, tutapambana ili kuweza kupata matokeo mbele ya
changamoto hizo, sikupenda kukutana na Yanga katika hatua za mwanzoni,
lakini ndiyo imeshakuwa hivyo.”
Katika Kagame ya msimu huu, Azam ndiyo yenye
rekodi ya kuvutia ikiwa imeshinda mechi zake zote za makundi na
haijafungwa hata bao moja. Pia safu yake ya ushambuliaji inatisha kwa
kufunga mabao manane. Ndiyo yenye wastani mzuri kati ya timu 13
zinazoshiriki.
Mechi ya kesho pale Uwanja wa Taifa itakuwa ya nne
katika michuano ya Kagame. Ni pambano gumu litakalokuwa na upinzani
mkali na Hall anaamini kuwa moto walioanza nao kwenye michuano hiyo
ndiyo utakaowachoma na Yanga.
Lakini kocha wa Yanga, Hans van Pluijm, amesema
hatishwi na rekodi tamu za Azam, badala yake amekiandaa kikosi chake kwa
mechi ya nusu fainali kwani ana hakika ya ushindi katika mchezo huo.
Pluijm alisema hatishiki na rekodi ya Azam ambayo
katika mechi tano za mwisho walizokutana nao Jangwani wamecheka mara
moja, badala yake akawahamasisha mashabiki wa Yanga kujiandaa
kusherehekea ushindi mapema.
Kocha huyo Mdachi alisema anafahamu kuwa mchezo
huo utakuwa mgumu kutokana na timu hizo mbili kufahamiana na kucheza
michezo mingi pamoja, lakini ana imani kubwa kikosi chake kitashinda na
kutinga hatua ya nusu fainali.
Yanga imelazimika kukutana na Azam katika hatua
hiyo baada ya mabingwa hao watetezi wa Ligi Kuu Bara kumaliza wakiwa
washindi wa pili wa Kundi A wakati Azam imemaliza ikiwa mshindi wa
kwanza wa Kundi C.
Mechi hiyo inakuwa ni marudio ya fainali ya Kombe
la Kagame ya mwaka 2012 ambapo Yanga ilishinda kwa mabao 2-0 na nyota wa
mchezo huo akiwa Said Bahanuzi aliyetemwa na Yanga hivi karibuni baada
ya Pluijm kudai kwamba ana masihara uwanjani.
Pluijm aligoma kuweka wazi mfumo atakaoutumia
katika mchezo huo kuikabili Azam ambayo inatumia mfumo wa 3-5-2 ambao
umeiwezesha timu hiyo kushinda mechi tatu mfululizo bila kuruhusu bao
hata moja.
“Kuhusu mfumo nitakaotumia siwezi kusema, hiyo itakuwa ni siri yetu,” alisema
Kipa wa Yanga, Ally Mustapha ‘Barthez’ amewataka
wachezaji wote wa timu hiyo kuwa makini kwani Azam siyo timu ya kubeza
na lolote linaweza kutokea katika mchezo huo.
- Mwanaspot
- Mwanaspot
إرسال تعليق