Tiffah wa Diamond apewa Benz la mil. 200!


Kazi ipo mwaka huu! Ndugu wa mzazi mwenzake na Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’ wamempa zawadi mtoto wa mastaa hao, Latiffah Nasibu ‘Princess Tiffah’ ndinga aina ya Mercedes Benz MSL Benz lenye thamani ya dola 100,000 (zaidi Sh. milioni 200).

Habari za uhakika kutoka ndani ya familia ya Diamond zilieleza kwamba, ishu hiyo ilijiri juzikati mara tu baada ya Zari ambapo baadhi ya ndugu wa mwanamama huyo walichanga na kumletea Tiffah gari hilo ili Zari alitumie katika mishemishe zake anapotoka na mwanaye Tiffah ikiwa ni pamoja na kumpeleka kliniki.

Kikisherehesha kwa kina stori hiyo, chanzo hicho kiliweka bayana kuwa ndugu wa Tiffah wameamua kumletea gari hilo ikiwa ni moja ya zawadi ambazo waliahidi kipindi akiwa majamzito, lakini pia wameamua kufanya hivyo kwa kuwa hawataki mtu achangie gari na Tiffah.

“Ni kweli ndugu wa Zari wameamua kumnunulia Tiffah gari aina ya Benz na tayari limewasili Bongo na Ijumaa iliyopita lilitumika kumpeleka Tiffah kliniki,” kilisema Chanzo hicho cha ndani.

Post a Comment

Previous Post Next Post