Wapenda vipodozi,hivi serikali imesema ni hatari usinunue vimeingia kimakosa sokoni

 Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Hiiti Sillo (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari Makao Makuu ya TFDA Dar es Salaam leo, wakati akitoa tahadhari ya uwepo katika soko wa vipodozi vyenye viambato vilivyopigwa marufuku na Serikali. Kulia ni Mkurugenzi wa Dawa  na Bidhaa Nyongeza, Fimbo Mitungu.
 Mkurugenzi wa Dawa  na Bidhaa Nyongeza, Fimbo Mitungu (kushoto), akizungumza katika mkutano huo huku akionesha moja ya kopo lenye kipodozi vilivyopigwa marufuku. Kulia ni Kaimu Mkurugenzi Uendelezaji Hudumawa TFDA, Chrispin Severe 
Baadhi ya vipodozi hivyo ambavyo vina madhara kwa matumizi ya binadamu
Mamlaka ya chakula na dawa nchini Tanzania TFDA leo wametangaza uwepo wa aina ya vipodozi aina 36 ambazo ni feki na ni hatari kwa matumizi ya binadamu na kuwataka wananchi kuwa makini katika kununua aina hiyo.

Akizungumza na wanahabari leo Jijini Dar es salaam mkurugenzi  wa TFDA Hiiti Sillo amesema kuwa wanautaarifu umma kuwa kupitia mfumo wake wa ufwatiliaji ubora na usalama wa bidhaa kwenye soko imebaini uwepo wa vipodozi vyenye viambato vilivyopigwa marufuku aina ya STEROIDS zinazojulikana kitaalam kama CLOBETASOL PROPIONATE,HYDROCORTISONE na TRIAMCINOLONE.

Amesema kuwa aina ya vipodozi tofauti 36 vya jamii ya krimu na losheni vimebainika kuwa na viambato hivyo vilivyopigwa marufuku baada ya kufanya uchunguzi wa kina wa matoleo 57 yaliyochukuliwa kwenye soko na viwanda vinavyotengeneza.

Vipodozi hivyo vimetengenezwa na makampuni manne yaliyopo nchini Tanzania na kampuni moja kutoka nchini Africa kusini.makampuni hayo ni 

–CHEMI-COTEX INDUSTRIES LIMITED-DAR ES SALAAM
-MAMUJEE PRODUCT LIMITED-TANGA

-TANGA PHARMACEUTICAL AND PLASTICS LIMITED-TANGA

-TRIDEA COSMETICS LIMITED-DAR ES SALAAM

-JOHNSON AND JOHNSON LIMITED –AFRICA KUSINI.

Amesema kuwa baadhi ya madhara makubwa yatikanayo na vipodozi hivyo ni pamoja na kuvimba mwili,muwasho,ngozi kiwaka moto,ngozi kukatika katika,ngozi kubabuka,kuwa nyeupe isiyokuwa ya kawaida,madhara kwenye mifupa,kizunguzungu,pamoja na madhara mengine mengi ikiwemo kiznguzungu na kichwa kuuma.

Baada ya kugundua dawa hizo kuwepo sokoni TFDA imezuia kwa muda wa mkiezi sita utengenezaji wa vipodozi aina ya krimu,losheni,na jeli kwenye viwanda vinne ambavyo vimekutwa na makosa hayo.

Wenye viwanda hivyo wameelekezwa kuviondoa vipodozi hivyo sokoni na kuviteketeza kwa gharama yao.
TFDA imefuta usajili wa vipodozi 31 vilivyokuwa vimesajiliwa.
Pia ukaguzi zaidi kutoka kwa mameneja wa TFDA ili kubaini aina nyingine ya bidhaa zilizopo sokoni ambazo sio nzuri kwa mwanadamu.

Post a Comment

Previous Post Next Post