Washiriki wa shindano la Mama Shujaa wa Chakula 2015 watinga kambini kijiji cha Makumbusho jijini Dar

 
Bi. Sophia Mkazi na Mwenyeji wa Kijiji cha Kasanga Wilayani Kisalawe Mkoani Pwani akiwakaribisha wageni ambao ni Washiriki wa Shindano la mama shujaa wa Chakula kijijini huko katika sherehe ya  iliyofanyika Kijiji cha Makumbusho Jijini Dar es salaam Jana. ambapo Programu mzima itaoneshwa katika Runinga ya ITV kila Siku kuanzia Tarehe 2.08.2015-21.08.2015 kuanzia saa 12 Jioni.
Bw. Godia Kaimu Mwenyekiti wa Kijiji cha Kasanga akiwakaribisha washiriki wa Shindano la Mama shujaa wa Chakula Shindano Linaloendeshwa na Oxfam Tanzania kupitia Kampeni ya Grow Kijijini kwake.
Kaimu Mkurugenzi Mtendaji Wilaya ya Kisalawe Bw. Ellioth Phillemon akiwakaribisha washiriki wa shindano la Mama Shujaa wa Chakula Wilayani Kisarawe.
Kikundi cha Burudani na sanaa cha  Rumumba Theatre wakiendelea na Burudani wakati wa sherehe hizo za ukaribisho kijiji cha Makumbusho.
Eluka Kibona, Meneja Utetezi na Ushawishi wa Oxfam akielezea kwa ufupi juu ya Mchakato mzima wa Shindano la Mama shujaa wa chakula ambalo linalenga kuwawezesha wakina mama kutambulika katika kilimo na kueleza Matakwa yao juu ya kilimo endelevu.
Bi. Mwanaidi Hamza ambaye anatoka katika Programu ya Big Result now akitoa ushuhuda jinsi gani alivyofanikiwa kulingana na Proramu hiyo na sasa anamaisha mazuri, na kuwasihi wakina mama wasikate tamaa katika kilimo.
Mkurugenzi Msaidizi Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Bw. Jackson Samwel akiwapongeza Shirika la Oxfam kupitia kampeni yake ya Grow kuanzisha shindano la Mama shujaa wa Chakula , kwa kutambua umuhimu wa ardhi katika kuzalisha chakula, ameshauri akinamama wabadilishane uzoefu pindi watakapokuwa kambini ili kuja na mbinu mpya za kilimo, ufugaji na uvuvi.
Mmoja wa watoa Burudani, Mwanamke huyu akionesha kuhusu swala zima la Kilimo Endelevu.
Stephen Mfuko aka Zero akitaja namba za washiriki na Jinsi ambavyo wanaweza Pigiwa Kura  ambapo Programu mzima itaoneshwa katika Runinga ya ITV kila Siku kuanzia Tarehe 2.08.2015-21.08.2015 kuanzia saa 12 Jioni.
60
Wageni waalikwa katika sherehe hiyo.
 
Ofisa wa Programu ya Kampeni ya Grow Tanzania Suhaila Thawer akitoa maelezo mafupi ya Mchakato rasmi wa kumsaka Mshindi wa Mama shujaa wa Chakula.
Wanao onekana Mbele ni Baadhi ya wenyeji ambao ndio watakuwa wenyeji wa washiriki wa mama shujaa wa chakula pindi watakapokuwa kijijini.
Mkurugenzi Mkazi wa Oxfam Tanzania Jane Foster akiwashukuru wadau mbalimbali ambao wamefanikisha mchakato mzima wa kuendesha shindano la Mama Shujaa wa Chakula, pia kipekee amewashukuru wafanyakazi wa Oxfam akiwepo Eluka Kibona na Suhaila Thawer kwa kuwa mstari wa mbele kufanikisha shindano hili na mwisho kuwatakia kila la heri washiriki wote wanaokwenda katika kushindana kumpata Mama Shujaa wa Chakula.
Washiriki wa Shindano la Mama shujaa wakiwa wanatambulishwa tayari kuelekea Kisarawe Kijiji cha Kisanga kwa ajili ya kumsaka mshindi ambapo Programu mzima itaoneshwa katika Luninga ya ITV kila Siku kuanzia Tarehe 2.08.2015-21.08.2015 kuanzia saa 12 Jioni
Picha Na MoBlog

Post a Comment

Previous Post Next Post