Kesi Ya UKAWA Imefunguliwa ICJ Sio ICC

 NI ICJ SIO ICC.!

Kuna watu wamekua wakihoji iweje viongozi wa UKAWA waende ICC wakati hakuna makosa yoyote ya uhalifu wa kivita yaliyotokea nchini? Wengi wanaoongea hivi ni CCM na wanaonekana wazi kuwa wako missinformed. Mara nyingi CCM huwa wanajenga hoja bila kuwa na taarifa za kutosha. (Elimu, Elimu, Elimu).!

Jibu sahihi ni kwamba viongozi wa UKAWA hawajaenda ICC wameenda ICJ. Hizi ni mahakama mbili tofauti zenye jurisdiction tofauti japo zipo mji mmoja wa The Hague.

The Hague kuna mahakama mbili. Ya kwanza ni mahamaka ya uhalifu wa kivita na makosa yatokanayo na vita vya kisiasa (Internation Criminal Court au ICC kwa kifupi). Ya pili ni mahakama ya kimataifa ya haki za raia (International Court of Justice, au ICJ kwa kifupi).

So kina Mbowe wameenda ICJ sio ICC. Wangeenda ICC ikiwa Serikali ingehusika na mauaji ya raia wakati wa uchaguzi. Lakini kwa kuwa hakuna uhalifu wa kivita uliotokea thats why wameenda ICJ.

ICJ inashughulikia mambo mengi ikiwa ni pamoja na issues za malalamiko ya uchaguzi. Kwa mujibu wa Article 93 ya UN Charter, nchi zote wanachama wa UN ni member wa mahakama hii. Na raia wa nchi hizo wanaweza kufile kesi kuhusiana na ukiukwaji wa haki za raia katika nchi zao, ikiwa ni pamoja na mambo ya uchaguzi.

 KWANINI ICJ?

Iko hivi wakati tunavunja mkataba wa Richmond tulishtakiwa ICJ tukashindwa kesi na hadi leo tunalipa hasara iliyotokana na kuvunja mkataba ule. Na sio Richmond tu zipo kesi nyingi tumewahi kushtakiwa ktk mahakama za kimataifa na tukashinda au kushindwa na tukatekeleza hukumu iliyotolewa.

Hivyo basi ili kulinda amani ya nchi Lowassa amefungua kesi ktk mahakama hiyo kudai kuporwa ushindi. Jana ametakiwa kupeleka "documents" za kudhibitisha madai yake na zilipelekwa jana na jopo la mawakili wa chama akiwemo John Mallya.

Kutokana na vielelezo vya Chadema, mahakama hiyo ilijiridhisha kuwa kuna kesi ya kujibu. Hivyo imewaagiza CCM nao kupeleka vielelezo vyao vinavyoonesha kuwa wameshinda kihalali (yani nakala zote za fomu za matokeo ktk majimbo ya uchaguzi kama ilivyofanya UKAWA).

Leo CCM imepeleka jopo la mawakili nchini Uholanzi kwa ajili ya kuwasilisha utetezi wake. UKAWA nao wataongeza mawakili wengine jioni ya leo akiwemo Tundu Lissu.

Tume ya Uchaguzi (NEC) kama sehemu ya walalakiwa ktk shauri hili nayo itawasilisha utetezi wake mbele ya mahakama hiyo chini ya jopo la majaji watatu kutoka serikalini.

Taarifa zisizo rasmi zinasema kesi hiyo itaanza kusikilizwa kesho na hukumu kutolewa kabla Rais mpya wa Tanzania hajaapishwa (November 05).

Pamoja na mambo mengine mahakama hiyo itapitia upya fomu zote za matokeo ktk majimbo yote kutoka NEC pamoja na zile zilizowasilishwa na CHADEMA na CCM ili kubaini kama kulikua na udanganyifu.

NB;
Mahakama hii haina mandate ya kumvua Magufuli ushindi (kuyokana na Katiba yetu ibara ya 41(7) kuzuia. Ila jurisdiction ya Mahakama hii ni kusema kama kuna udanganyifu ulifanyika au lah. Mahakama hii pia inaweza kueleza kama kuna njama za kuhujumu matokeo (conspiracy) zilizofanywa baina ya CCM na Tume ya Uchaguzi. Kwahiyo hata km mahakama hii haiwezi kumvua Magufuli ushindi, lakini hukumu yake inaweza kusababisha uchaguzi urudiwe kama ilivyofanya kwa nchi ya Romania miaka iliyopita.

MY TAKE.!

Hii imedhihitisha kuwa Lowassa ni kiongozi wa kipekee (Charismatic Leader). Anajua watu wana uchungu na ubakaji wa demokrasia uliotokea. Anajua neno lake moja tu linaweza kufanya mamilioni ya watanzania wakakusanyika barabarani bila kuhofia kupoteza maisha yao. Anajua kuwa ana nguvu na uwezo wa kuitisha maandamano nchi nzima na vyombo vya dola vikashindwa kuzuia hata vikiua baadhi. Anajua kwa nguvu aliyonayo anaweza kupelekea taifa hili likaingia kwenye machafuko makubwa.

Lakini badala ya kufanya hivyo ameamua kutumia njia za kistaarabu kudai haki yake. Ameamua kwenda Mahakamani. Kwangu hii ni sifa ya kiongozi bora wa karne. Naanza kuelewa kwanini alisisitiza ELIMU, ELIMU, ELIMU. Lowassa anapenda Elimu, anatamani watu wapate Elimu, Lowassa anaiishi Elimu. May GOD in Trinity bless him abundantly.!

Chanzo...Jamii Forum

Post a Comment

Previous Post Next Post