Jitihada
za serikili kwenye mapambano dhidi ya ujangili zinaendelea kuzaa
matunda baada ya Kikosi cha Kupambana na Ujangili kumkamata mtuhumiwa
mkuu wa ujangili anayejulikana kama Shetani.
Kukamatwa
kwa jangili huyo kumetokana na jitihada za usiku na mchana zilizofanywa
kwa ushirikiano wa Wizara ya Maliasili na Utalii na wadau wengine
hususan askari wa wanyamapori kwa kipindi cha mwaka mmoja kwenye maeneo
mbalimbali ya uhifadhi nchini.
Akizungumza
wakati akielekea jijini London, Uingereza kwa safari ya siku mbili ya
kikazi, Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, alisema kazi
iliyofanyika ni kubwa na inastahili pongezi.
Alisema
majangili wamekuwa wakiisumbua serikali kwa kipindi kirefu lakini
kutokana na jitihada za serikali na wadau wengine zikiwemo nchi wahisani
wa maendeleo na jumuia za kimataifa hali inaendelea kuwa nzuri.
Alisema
Shetani anakuwa wa pili kukamatwa baada ya Queen of Victory aliyekamatwa
na serikali kipindi cha nyuma akiendelea na jitihada za kufanya uhalifu
wa kuua na kuiba viungo vya wanyamapori wa Tanzania.
Waziri
Nyalandu alisema serikali itaendelea na mapambano ya kuwasaka na
kuwachukulia hatua za kisheria vigogo wa ujangili na wanaowasaidia
kufanikisha uhalifu huo hapa nchini.
Alisema
akiwa jijini London atahudhuria mkutano wa Mawaziri wa Utalii kutoka
nchi mbalimbali zikiwemo za Afrika Mashariki, ambao watazungumza mambo
mbalimbali yanayohusu namna za kuendeleza sekta ya Utalii katika ukanda
wa Afrika Mashariki.
Alisema
pia mkutano huo utahudhuriwa na Mwanahabari maarufu wa Shirika la Habari
la CNN, Richard Quest atakayefanya mahojiano maalumu kuhusu masuala ya
Utalii na Maliasili.
Kuhusu
hali ya siasa nchini, Nyalandu alisema uchaguzi umeisha na kwamba
viongozi walioshinda wanapaswa kufahamu kuwa si wao walioshinda bali ni
watanzania kwa ujumla hivyo wawe wamoja kuijenga Tanzania.
Post a Comment