Mmoja wa wachezaji wanaowania tuzo za Caf mwaka huu, Andrew Ayew..
Shirikisho
la Soka barani Africa limeyataja majina 10 ya wachezaji wanaowania tuzo
ya mchezaji bora barani Afrika kwa mwaka wa 2015. Katika majina hayo
pia ameorodheshwa mchezaji bora kwa mwaka 2014, Mchezaji wa timu ya
taifa ya Ivory Coast na klabu ya Mnachester City.
Kwa
upande wa taifa nchi ya Algeria na Ivory Coast yamefanikiwa kuingiza
wachezaji wawili kila moja kwa upande wa Algeria wachezaji ambao
wameingia katika orodha hiyo ni Sofiane Feghouli anayekipiga katika
klabu ya Valencia inayoshiriki Ligi kuu ya nchini Hispania (Primera
Division) na mchezaji mwingine ni Yacine Brahimi anayekipigiga katika
klabu ya Porto inayoshiriki Ligi kuu ya Ureno.
Kwa
taifa la Ivory Coast imemuingiza Serge Aurier anayekipiga katika klabu
ya Paris Saint-German inayoshiriki ligi kuu ya Ufaransa (Seria A) na
Yaya Toure anayechezea Manchester City inayoshiriki ligi ya Wingereza
(Primear League)
Wachezaji hao ni pamoja na Andre Ayew (Ghana-Swansea City), Aymen Abdennour ( Tunisia-Valencia), Mudather Eltaib Ibrahim (Sudan-Al-Hilal), Mohamed Salah (Egypt-Roma), Pierre-Emerick Aubameyang (Gabon-Dortmund), Sadio Mane (Senegal-Southampton), Serge Aurier ( Ivory Coast-Paris Saint-German), Sofiane Feghouli (Algeria-Valencia).
Pia wapi Yacine Brahimi (Algeria-Porto) na Yaya
Toure ambaye anashikilia tuzo hiyo aliyoitwaa mara mbili mfululizo
katika misimu miwili iliyopita akitokea Ivory Coast na klabu
ya Manchester City.
Post a Comment