GOOD news ikifukie kwako mpenda burudani kwamba baada ya kusumbua na Ngoma ya Nana ‘Sankoro’, King wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ jana (Ijumaa) kupitia mitandao, redio za ndani na nje ya nchi ameshusha ngoma yake mpya.
Ikumbukwe kuwa hadi sasa ngoma ya Nana
iliyotoka rasmi Mei mwaka huu ni moja ya ngoma kali za Diamond
zilizofanya vizuri na kumuongezea wigo wa soko la muziki ndani na nje ya
nchi.
Tuzo
Moja ya mafanikio aliyoyapata Diamond
mwaka huu kupitia Ngoma ya Nana ambayo kideo chake kimefanywa na Kampuni
ya Godfather nchini Afrika Kusini ni kuibuka na tuzo kibao kama vile
MTV Europe (EMA), African Muzik Magazine (Afrimma), Nollywood &
African Films Critics (Nafca) na nyingine kibao.
Rekodi
Kwa takriban mwaka mmoja, Ngoma ya Nana
imeweka rekodi katika mtandao wa Youtube kuwa miongoni mwa ngoma za
Diamond zilizotazamwa na mashabiki wake mara nyingi zaidi ikiwa ni mara
milioni 7,268,108.
Ngoma zake nyingine zilizotazamwa mara
nyingi ni Mdogomdogo iliyotoka mwaka jana ambayo imetazamwa mara
5,086,813. Nayo Ntampata Wapi iliyotoka Desemba mwaka jana imetazamwa
mara 6,597,653 pamoja na Nasema Nawe iliyotoka Aprili mwaka huu ambayo
imetazamwa mara 5,531,289.
Mashabiki wengi wa Diamond na Muziki wa
Bongo Fleva wanatarajia kuona ngoma ya leo ikiweka rekodi ya aina yake
kwa kusikilizwa na kutazamwa mara nyingi zaidi ndani na nje ya nchi
sambamba na kumletea mafanikio kama ilivyokuwa kwa Nana.
Akizungumzia ngoma mpya, Diamond alisema
kwanza itakuwa ni moja ya ngoma zake kali zote alizowahi kuzitoa. “Kama
ilivyo kawaida yangu sina maneno mengi, ngoma itajieleza yenyewe na hii
ni sapraizi kubwa kwa mashabiki wangu,” alisema Diamond.
Kuitambulisha Dar Live
Kwa mara ya kwanza baada ya kuachiwa
ngoma hiyo mpya, Diamond ataizindua rasmi Sikukuu ya Krismasi (Desemba
25) mwaka huu ndani ya Uwanja wa Taifa wa Burudani, Dar Live uliopo
Mbagala- Zakhem jijini Dar.
Ikumbukwe kuwa mara ya mwisho kwa
Diamond kufunika Dar Live ilikuwa Krismasi mwaka jana katika bonge moja
la shoo lililokuwa likitambulika kama Usiku wa Wafalme akiwa na Mfalme
Mzee Yusuf ambapo Diamond alikamua ngoma zake zote kali kama vile
Ntampata Wapi, Mdogomdogo na nyinginezo.
Katika kunogesha Sikukuu ya Krismasi Dar
Live, mbali na Diamond kukamua na madensa wake, bingwa wa muziki wa
Singeli, Msagasumu naye atakuwepo jukwaani kukamua ngoma zake zote kali.
Siku hiyo Msagasumu ataimba ngoma yake
iitwayo Inaniuma Sana aliyomshirikisha Nature, Huyo Mtoto, Shemeji
Unanitega, Naipenda Simba na nyingine kibao.
Mabingwa wa sarakasi, kucheza muziki wa kila aina, Wakali Dancers nao watakuwepo kukamilisha hamu ya mashabiki wa burudani.
Post a Comment